Saturday, August 6, 2016

AC MILAN YAUZWA KWA WACHINA

Katika hali ya kushangaza aliyekuwa Mmiliki wa klabu ya AC Milan, Silvio Berlusconi amewauzia wachina hisa zake zote ambazo ni asilimia 99.93.

Ripoti ya Gazzetta World inasema, Meneja uwekezaji Changxing, pamoja na wafanya biashara wengine wakubwa raia wa china, Li Yonghong wamelipa kiasi cha Euro milioni 740 kuinunua klabu hiyo, kiasi hicho cha fedha kikijumuisha deni ambalo klabu hiyo ilikuwa inadaiwa la Euro milioni 220.

Asilimia 0.07 ya hisa iliyobaki itakuwa inamilikiwa na familia ya Berlusconi, baada ya miaka 30 ya Waziri mkuu huyo wa zamani wa Italy kuimiliki klabu hiyo.
Ungana na Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA

0 comments:

Post a Comment