Thursday, June 2, 2016

YANGA YAPINGA TFF KUINGILIA UCHAGUZI WAO

Klabu ya Yanga imepinga suala la TFF kuonekana kuingilia uchaguzi wao na kusema wao watafanya uchaguzi wao wenyewe.




Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF lilitangaza kuwa mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Yanga unasimamiwa na Shirikisho hilo kwa mujibu wa utaratibu waliokautoa hapo awali, lakini klabu ya Yanga imeibuka na kusema wanapingana na kauli hiyo ya TFF na kwamba uchaguzi utasimamiwa na wao wenyewe na kamwe hawatoweza kukubali uchaguzi huo usimamiwe na TFF ambayo inajumuisha watu mbalimbali wengine wakiwa sio wanayanga.

TFF ilitoa tarehe ya uchaguzi wa Yanga kuwa ni Juni 6 lakini Yanga nao wametoa ratiba ya matukio yote ya uchaguzi huo na katika kalenda yao inaonyesha uchaguzi utafanyika Juni 11 badala ya 6 ambayo ilitangazwa na TFF.

Akizungumza na waandishi wa habari kaimu katibu mkuu wa klabu ya Yanga, Baraka Deudiet amesema kamati ya uchaguzi na bodi ya wadhamini imemwagiza kutangaza tarehe yao ambayo watafanya uchaguzi na sio ile ya TFF

"Nimepewa maelekezo na kamati ya uchaguzi ya Yanga na bodi ya Wadhamini kutangaza mchakato wa uchaguzi wa klabu yetu kama tulivyotakiwa na serikali kufanya hivyo baada ya kuwaandikia TFF lakini tunashangazwa na TFF hao kutangaza mchakato wa uchaguzi wetu kinyume na inavyotakiwa" alisema Baraka.


Related Posts:

  • VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports. Simba w… Read More
  • ACACIA KUSITISHA UDHAMINI NA STAND UNITED KAMPUNI ya ACACIA inayoidhamini timu ya Stand United ya mkoani Shinyanga imesema itaondoa udhamini wake na klabu ya Stand kama Stand itaendeshwa kama kampuni. Taarifa hizo zimekuja mara baada ya Stand kutangaza kuwa kwa … Read More
  • VICENT BOSSOU AITWA TIMU YA TAIFA YA TOGO Kocha mpya wa Togo Mfaransa Claude LeRoy amemuita Vicent Bossou katika kikosi cha timu yake ya Taifa .Bossou ameitwa kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha akiwa na klabu ya Yanga. Tayari barua ya mualiko wa kujiu… Read More
  • AMIS TAMBWE AMWOMBEA MABAYA KIIZA MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Dar Young Africans Amis Tambwe, amemaliza mchezo wa jana dhidi ya Ndanda FC bila ya kufunga goli, Tambwe anayeongoza katika orodha ya wafungaji bora katika ligi kuu Tanzania bara msim… Read More
  • TWITE NA BOSSOU WAANZA RASMI MAZOEZI Yanga wapo katika maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wao wa hatua ya mtoano kombe la shirikisho barani Africa dhidi ya Sagrada Esperanca ya Nchini Angola, wakati kikosi cha Yanga kikijiweka fiti kuukabili mchezo huo,… Read More

0 comments:

Post a Comment