Friday, June 10, 2016

YANGA KUANZA KAMBI RASMI LEO

Timu ya Dar Young Africans inatarajiwa kuingia kambini leo kujiandaa na michezo ya hatua ya makundi CAF Confederation Cup.


Yanga itacheza mchezo wake wa kwanza katika hatua hiyo Juni 19 dhidi ya MO Bejaia ya nchini Algeria, mchezo utakaopigwa huko Algeria majira ya saa 4 usiku kwa Algeria sawa na Saa 6 usiku saa za Afrika Mashariki.

Akizungumzia maandalizi hayo Meneja wa Yanga Hafidi Salehe amesema, wataweka kambi Dar Es Salaam na kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Taifa kwa ajili ya maadalizi hayo.

"Kesho (leo) tunatarajia kuingia kambini Dar Es Salaam kwa ajli ya maandilizi ya michuano ya kombe la shirikisho Afrika, kujiimarisha na kuhakikisha tunajiweka sawa kwa mazoezi tayari kwa mchezo wetu wa kwanza tutakaocheza" alisema Meneja huyo.

Wachezaji wote wa Yanga wapo kikosini hapo isipokuwa Vicent Bossou ambaye anatarajiwa kuwasili wakati wowote akitokea kwao Togo. Salehe alisema kiujumla maandalizi yao yanakwenda vizuri na kwamba uchaguzi unaoendelea Yanga hauwezi kuathiri mipango yao ya kujiandaa kwenda kuwakilisha vyema katika michuano hiyo.

Related Posts:

  • NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu … Read More
  • MSIMAMO KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRIKA CAF CC Msimamo Kombe La Shirikisho Barani Afrika 2016 (CAF CC) … Read More
  • YANGA KULIPA ZAIDI YA MILION 500 CAFKlabu ya Yanga imetakiwa kulipa fidia ya Tsh. milioni 530 kama fidia ya gharama za mchezo wao dhidi ya TP Mazembe baada ya kuruhusu mashabiki kuingia bure uwanjani. CAF na TFF imefikia hatua hiyo baada ya Yanga kufuta kiin… Read More
  • MEDEAMA KUTUA DAR KESHO Wapinzani wa Yanga katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika, Medeama ya Ghana wanatarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa mchezo wa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga katika msimamo wa Kund… Read More
  • KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA TP MAZEMBEKIKOSI CHA YANGA LEO. 1. Deogratius Bonaveture Munishi 'Dida' 2.Juma Abdul Mnyamani. 3. Mbuyu Twite Junior. 4. Kelvin Patrick Yondani "Cotton" 5. Vicent Bossou. 6. Thaban Michael Kamusoko. 7. Juma Mahadhi. 8. Haruna Fadhil… Read More

0 comments:

Post a Comment