Sunday, June 12, 2016

UJIO WA NYOTA HUYU YANGA WAMWEKA ROHO JUU TAMBWE

Mshambuliaji wa Yanga Amiss Tambwe amesema hana hofu ya kupoteza nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza cha Yanga kufuatia ujio wa wachezaji wapya Yanga.
Walter Musona

Yanga inakaribia kuinasa saini ya mshambuliaji hatari kutoka nchini Zimbabwe, Walter Musona ambaye anamudu kucheza nafasi ya Tambwe.

Kwa upande wake Tambwe amesema hana hofu yoyote ya kupoteza namba katika kikosi cha kwanza Yanga lakini akikiri kuwa soka ni mchezo wa ushindani hivyo kujituma kwake ndo kutamhakikishia nafasi klabu hapo.

Tambwe
"Soka ni mchezo wa ushindani kwa timu na timu, wachezaji kwa wachezaji, kama mchezaji siku zote nipo kwa ajili ya kuisaidia timu yangu, lakini pia ushindani kutetea nafasi yangu uwanjani" alisema Tambwe.

"Nawakaribisha wachezaji wapya kwa ajili ya kuipigania Yanga, lakini hitakuwa rahisi kupoteza nafasi yangu." aliongeza.

Tambwe alijiunga na Yanga akitokea Simba na amekuwa na uzoefu mkubwa katika ligi kuu Vodacom huku akifanikiwa kutwaa tuzo ya mfungaji bora wa ligi hiyo msimu huu kwa kufikisha jumla ya magoli 21 katika ligi.
==============
 Bonyeza hapa ku-Like Page yetu ya Facebook
==============

Related Posts:

  • LIVE KUTOKA TAIFA - FUATILIA LIVE MCHEZO KATI YA SIMBA NA TOTO AFRICANS HALF TIME MATOKEO: SIMBA 0 - 1 TOTO AFRICANS Mfungaji: Wazir Junior  ======== KIPINDI CHAPILI KIMEANZA Dakika ya 47: beki wa Simba, Hassan Kessy anapewa kadi nyekundu kwa kumchezea faulo, Edward Chris… Read More
  • Hapatoshi Leo Tena Taifa Patashika za ligi kuu ya kandanda tanzania bara zinaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu kupigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha wenyeji Simba SC dhidi ya Toto Africans ‘wana kishamapanda’kutok… Read More
  • Mnyama Achinjwa Taifa Timu ya soka ya Simba imezidi kupoteza matumaini ya kunyakua ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kukubali kichapo cha Goli 1 - 0 toka kwa Toto Africans ya Mwanza.Katika mchezo huo ambao wadau wengi wa soka waliip… Read More
  • TFF Yatuma Salamu Za Rambirambi MZFA Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Mwanza (MZFA), kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti mstaafu wa MZFA na makamu mwenyekiti wa FAT Silvanus Maka… Read More
  • Tanzania Yazidi Kupata Umaarufu Duniani Bondia Ibrahim Class Bondia mtanzania Ibrahim Class ‘King Class Mawe’ameendelea kutamba katika mapigano yake nje ya nchi baada ya usiku wa kuamkia jana kufanikiwa kumtwanga Mjerumani huko Panama City Amerika Kusini. … Read More

0 comments:

Post a Comment