Sunday, June 12, 2016

TAARIFA YA MOURINHO YAWAGAWA MASHABIKI MAN U

Klabu ya Manchester United ilitangaza majina ya wachezaji wake ambao wataendelea kuitumikia United huku pia wakithibitisha kuwa nyota wanne hawana nafasi tena klabuni hapo.

Kiungo Nick Powell ni miongoni mwa wachezaji ambao wataondoka klabuni hapo huku taarifa ya kuondoka kwake ikipokelewa tofauti na mashabiki wa United.

Powell 22, alitabiriwa kuja kuwa mchezaji bora sana alipojiunga na United mwaka 2012, lakini amecheza mechi 3 tu katika kipindi cha miaka 4 kwenye ligi kuu nchini England na sasa Powell anajikuta akitupiwa virago klabuni hapo.

Taarifa za kuchukuliwa kwa mkopo katika klabu za Wigan Athletic, Leicester na Hull City nazo pia zimeonekana kutokuzaa matunda na kuonekana wazi kuwa maisha ya Powell katika soka kuingia matatani.



Hatahivyo mashabiki wa United wamekuwa na maoni tofauti kufuatia kuachiwa kwa Powell katika klabu hiyo,Wengi wakisema kinda huyo hakupewa nafasi ya kuonyesha uwezo wake.

Hizi hapa ni Tweets za mashabiki hao wakieleza hisia zao;





==============
 Bonyeza hapa ku-Like Page yetu ya Facebook
==============

Related Posts:

  • ROBERT LEWANDOWSKI KUTUA REAL MADRID Wakala wa Robert Lewandowski, Cezary Kucharski amethibitisha kuwa Real Madrid walimfuata kuhusu uwezekano wa Lewandowski kutua Bernabeu. Lewandowski aliye katika kiwango cha hali ya juu kwa hivi sasa anamaliza mkataba na… Read More
  • AL AHLY WAMNYATIA DONALD NGOMA Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe Donald Ngoma ameanza kuwindwana vigogo wa soka la Misri na Afria timu ya Al Ahly. Ngoma amekuwa mshambuliaji tishio sana katika klabu ya Yanga na ametoa mchango mkubwa sana katika ma… Read More
  • PAUL NONGA ANYOOSHA MIKONO YANGA Mchezaji aliyejiunga na Yanga akitokea Stand United Paul Nonga amesema ameuomba uongozi wa Yanga umuuze. Nonga amefikia uamuzi huo baada ya kukosa nafasi ya kucheza muda mwingi katika klabu hiyo. ”Nimeomba kuuzwa na tay… Read More
  • JOSE MOURINHO ATANGAZWA RASMI KUWA KOCHA WA MANCHESTER UNITED JOSE MOURINHO ametangazwa rasmi kuwa kocha mkuu wa Manchester United kwa mkataba wa miaka 3. Mourinho amechukua mikoba ya Louis Van Gaal na anakuwa kocha wa 25 kwa United. Hii hapa ni tweet ya akaunti rasmi ya Machester … Read More
  • KLABU 2 ZA MISRI VITANI KUWANIA SAINI YA DONALD NGOMA Klabu za Misri Al Ahly na Zamalek zipo katika vita ya kuwania saini ya Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma. Uwezo mkubwa wa Donald Ngoma anapokuwa uwanjani umezifanya klabu nyingi kuhitaji saini ya mchezaji huyo anaeitumi… Read More

0 comments:

Post a Comment