Thursday, June 23, 2016

NGASSA AUKUBALI MZIKI WA YANGA

Mrisho Ngassa Mtanzania anayechezea klabu ya Free State ya nchini Afrika Kusini amepongeza uwezo mkubwa waliouonyesha Yanga kwenye mechi yao dhidi ya MO Bejaia.

Ngassa ambaye yupo likizo kwa sasa amesema Yanga walicheza vizuri sana katika mchezo huo huku akisema kilichowaangusha ni kushindwa kuzitumia nafasi nyingi za magoli walizozitengeneza kwenye mchezo huo.

"Walicheza vizuri sana na walitengeneza nafasi nyingi lakini kwa bahati mbaya tu walishindwa kuzitumia nafasi hizo kufunga magoli. Walipambana hadi dakika za mwisho wakitaka kusawazisha goli hilo, kilikuwa ni kiwango kizuri sana." alisema Ngassa mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga.

Yanga sasa ina kibarua kizito dhidi ya TP Mazembe mchezo utakaopigwa Jijini Daresalaam Juni 28, 2016.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • TAZAMA MASHABIKI WA SIMBA WALIVYOLIANZISHA MSIMBAZI Kufuatia matokeo mabaya yanayoikumba klabu ya Simba katika mechi zao za hivi karibuni, mashabiki na wanachama wa klabu hiyo wameshindwa kuvumilia na kuamua kujikusanya katika makao makuu ya klabu hiyo kwa kile wanachodai … Read More
  • HASSAN RAMADHANI KESSY AMWAGA WINO YANGA Beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za Mkataba wa Yanga, Kessy amesaini miaka miwili kuitumikia Yanga kuanzia mwezi ujao. Zoezi hilo lilifanyika juzi usiku mjini Dar… Read More
  • HIKI NDO KIKOSI CHA SERENGETI BOYS Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi amewataka wachezaji wa timu ya soka ya vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kama jina la Serengeti Boys kwenda kucheza soka la ushi… Read More
  • TFF YAZIKUMBUSHA TENA KLABU ZA LIGI KUU 2016/17 Kwa mara nyingine, Bodi ya Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka (TFF) imezikumbusha klabu zitakazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2016/17 kuwa mchakato wa wa utengenezaji kanuni umeanza tangu Mei 5, 2016. Bodi ya Ligi… Read More
  • SIMBA YAIFUATA MAJIMAJI SONGEA Kikosi cha Simba kimesafiri alfajiri ya leo kuelekea Songea tayari kwa mchezo wake dhidi ya Majimaji FC. Simba itaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wake wa awali dhidi ya Mwadui FC, hivyo kuh… Read More

0 comments:

Post a Comment