Thursday, June 23, 2016

MATUMAINI YA CANNAVARO KUELEKEA MCHEZO NA MAZEMBE

Nahodha wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub Cannavaro anaamini kuwa kikosi chao kitatinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho Barani (CAF CC).

Yanga ambayo imepoteza mchezo wake wa kwanza kwa kukubali kipigo cha goli moja kwa bila kutoka kwa MO Bejaia ya nchini Algeria, itashuka dimbani tena kucheza na mabingwa wa Afrika timu ya TP Mazembe ya Congo DRC.

Cannavaro alikosa mchezo wa kwanza dhidi ya MO Bejaia kutokana na kutumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo wa kufuzu hatua ya makundi dhidi ya Sagrada Esperanca ya nchini Angola, Nahodha huyo amefurahishwa na kiwango walichokionyesha Yanga katika mchezo na Mo Bejaia licha ya kufungwa goli hilo moja.

"Naweza kusema tulikosa bahati katika mchezo ule kwa sababu timu ilicheza vizuri na tulitengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini tulishindwa kuzitumia na hicho ndicho kinanipa imani kama Yanga inaweza kucheza nusu fainali hata fainali mwaka huu" alisema Cannavaro.

Aidha Nadir alisema mipango yao ni kufanya mazoezi yakutosha ili kuikabili TP Mazembe, mchezo utakaochezwa Juni 28.

"Kocha Hans Pluijm na wenzake wa benchi la ufundi watakuwa wameona udhaifu wetu katika mchezo uliopita, hivyo watafanyia kazi kwenye mazoezi yetu kuelekea mchezo na Mazembe" aliongeza Nahodha huyo.

Yanga imeomba kwa shirikisho la soka Tanzania TFF kuiandikia barua CAF kuomba mechi yao na Mazembe ichezwe Juni 29 saa moja na nusu usiku badala ya Juni 28 saa 10:00 jioni.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • Yaliyojiri Uwanja Wa Taifa Leo Kati Ya Yanga Na Al Ahly Waamuzi Wa Mechi Ya Yanga na Al Ahly Leo Ile mechi ya klabu bingwa Afrika ikiyosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka kati ya Yanga ya Tanzania na Al Ahly kutoka Misri imemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya 1 - 1. … Read More
  • Ndanda Kosovo Afariki Dunia Ndanda Kosovo Enzi Za Uhai Wake Mwananamuziki maarufu wa dansi nchini, Ndanda Kosovo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Taarifa zinazotufikia, zinaeleza Ndanda amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa tumbo. … Read More
  • Kipre Tchetche Azifukuzia Rekodi Za Mbwana Samatta Ufungaji Bora CAF MSHAMBULIAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Kipre Tchetche, ameingia kwenye orodha ya wachezaji wanne wanaofukuzia ufungaji bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwaka huu. Tchetche ameingia … Read More
  • Farid Na Messi Waikalisha Esperance De Tunis Azam fc imefanikiwa kuichapa timu ya Esperance kutoka nchini Tunisia kwa mabao mawili kwa moja. Esperance walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 33 ya mchezo kupitia kwa mchezaji wake Haithem Jouini. Hadi timu zinakwenda m… Read More
  • Kiiza Yamkuta Tena Afukuzwa Kambini SimbaKOCHA wa Simba, Jackson Mayanja sasa ameingia kwenye ugomvi mkubwa na Mganda mwenzake, mshambuliaji Hamisi Kiiza. Mayanja amemfukuza Kiiza kambini Ndege Beach, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kwa shutuma za utovu wa nidha… Read More

0 comments:

Post a Comment