Wednesday, June 1, 2016

KIPRE TCHETCHE AOMBA KUONDOKA AZAM FC

Kipre Tchetche mchezaji wa Azam FC raia wa Ivory Coast amesema inatosha sasa kucheza Tanzania hivyo anataka kwenda kujaribu sehemu nyingine.




Kipre ambaye ana mwaka mmoja umebaki katika mkataba wake ametosheka na muda aliokaa nchini akicheza ligi kuu Vodacom. Kipre ameyasema hayo akiwa kwao nchini Ivory Coast alikokwenda kwa mapumziko.

"Inatosha kwa muda ambao nimecheza Tanzania, nahitaji kuondoka kwenda kutafuta changamoto nyingine kwingine. Nimekuwa na maisha mazuri sana Azam, viongozi na wamiliki wanajali sana wachezaji, lakini nalazimika kuyaacha yote" alisema Tchetche alipozungumza na Bin Zubeiry.

Kipre Tchetche yupo nchini Ivory Coast kwa mapumziko na tetesi zinasema nyota huyo ameshasaini mkataba na klabu moja ya Uarabuni.

Related Posts:

  • MURO ASEMA HUU NI WAKATI WA UZALENDO Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga watakuwa kibaruani Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwavaa Al Ahly kutoka Misri katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Tayari wachuuzi, wameanza kuuza jez… Read More
  • Azam Fc Yazuiwa Kuvuka Barabara Mvomero Mkoani Morogoro BARABARA ya Kijiji cha Mvomero, mkoani Morogoro ililazimika kutopitika kwa takribani dakika 15 kufuatia mashabiki wa soka wa kijiji hicho kujazana kwa wingi na kufunga barabara hiyo wakati wakiipokea Azam FC iliyotoka kuic… Read More
  • Kapombe Kutua Bongo BEKI kisiki wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shomari Kapombe, amerejea nchini jana jioni baada ya wataalamu wa Hospitali ya Morningside Mediclinic ya jijini Johannesburg, Afrika Kusini kurishidhwa na … Read More
  • Tambwe Amechuja Awekwe Benchi Mashabiki wa Klabu ya Dar Young Africans wameonyesha kutokufurahishwa na kiwango kinachoonyeshwa na mshambuliaji wao Amis Tambwe siku za hivi karibuni. Tambwe ambe ana magoli 18 katika orodha ya wafungaji bora msimu huu an… Read More
  • Abdi Banda Alia Na Viongozi Wa Simba Mchezaji wa Simba Abdi Banda anasema hajui mustakabali wake katika Klabu hiyo kufuatia tamko la adhabu aliyopewa kutokana  na kupishana kauli na kocha wake Jackson Mayanja katika mechi dhidi ya Coastal Union. Ana… Read More

0 comments:

Post a Comment