Wednesday, June 1, 2016

AL AHLY WAMNYATIA DONALD NGOMA

Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe Donald Ngoma ameanza kuwindwana vigogo wa soka la Misri na Afria timu ya Al Ahly.




Ngoma amekuwa mshambuliaji tishio sana katika klabu ya Yanga na ametoa mchango mkubwa sana katika mafanikio waliyoyapata  Yanga msimu huu. Amefunga jumla ya mabao 17 katika msimu wa ligi kuu Vodacom 2015/16, huku pia akiwafunga Al Ahly katika mchezo wa klabu bingwa Afrika uliochezwa Misri.

Al Ahly wameonyesha kuvutiwa na nyota huyo na kwamba wapo tayari kuingia sokoni kuiwinda saini yake mwishoni mwa msimu huu.Mapharao hao wanafikia hatua hiyo ya kumuhitaji Ngoma kufuatia wachezaji wao John Antwi wa Ghana na Malick Evouna wa nchini Gabon kushindwa kuonyesha kiwango bora.

Donald Ngoma mwenyewe ameonyesha utayari wake endapo Al Ahly watatuma ofa ya kumuhitaji katika klabu yao.

"Kwanini Hapana?, Ni klabu kubwa katika Afrika na nitakuwa tayari kwenda Misri" alisema Ngoma alipohojiwa na Marwan Ahmed wa Kingfut.com.

Yanga watakuwa na kibarua kizito cha kusaka mbadala wa Ngoma endapo wataamua kumuuza kwa Mapharao kwani amekuwa ni kivutio na mchango mkubwa katika klabu yao.

Related Posts:

  • SAKATA LA KESSY YANGA HATIMA YAKE LEOSuala la beki wa Kulia wa Yanga, Hassan Ramadhan "Kessy" kucheza mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya TP Mazembe  itafahamika leo baada ya kamati ya utendaji Simba kukutana. Yanga iliwaandikia Simba barua kutaka kuj… Read More
  • KOCHA PRISONS APANIA KUIBOMOA MTIBWA SUGARKocha Mkuu wa klabu ya Tanzania Prisons Salum Mayanga amesema anajipanga kuhakikisha anaibomoa Mtibwa Sugar kwa kuwasajili wachezaji muhimu wa kikosi hicho. Mayanga amepanga kumsajili mlinda mlango Hussein Sharifu kwa ajil… Read More
  • KOCHA MPYA SIMBA APEWA RUNGU LA KUSAJILI WAKIMATAIFASimba ipo mbioni kukamilisha usajili wa kocha Joseph Omog na tayari imeshampa ruksa kocha huyo kusajili wachezaji wakimataifa. Taarifa kutoka ndani ya klabu ya Simba ni kwamba kocha huyo anatarajiwa kutua muda wowote kuanz… Read More
  • ANTOINE GRIEZMANN AONGEZA MKATABA ATLETICOMshambuliaji wa klabu ya Atletico Madrid, Antoine Griezmann amesaini mkataba mpya na klabu ya Atletico Madrid utakaomuweka klabuni hapo hadi 2021. Griezmann alikuwa akihusishwa na kujiunga na vilabu vya ligi kuu ya Uingere… Read More
  • KIPA AONDOKA CHELSEA KWA MKOPAMlinda Mlando wa Chelsea Mitchell Beeney ameondoka klabu hapo kwa mkopo na kujiunga na klabu inayoshiriki ligi daraja la kwanza ya Crawley. Beeney 20, hajawahi kucheza mechi yoyote ya ligi kuu tangu ajiunge na Chelsea na m… Read More

0 comments:

Post a Comment