Sunday, June 26, 2016

HATIMAYE TAMBWE AFUNGUKA UJIO WA CHIRWA YANGA

Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe amesema kucheza timu kubwa kama Yanga kunahitaji ujasiri kutokana na usajili unaofanywa kila wakati.

Ujio wa mshambuliaji mpya kwenye kikosi cha Yanga, Mzambia Obrey Chirwa, unaonekana kutishia maisha ya Tambwe kwenye kikosi cha kocha Hans Pluijm, lakini mwenyewe amesema haitakuwa rahisi kama ambavyo watu wanadhani, kwani ataendelea kucheka na nyavu kama kawaida.

“Nitapambana uwanjani na kocha ndiye atakuwa na maamuzi, lakini nakubali Chirwa ni mchezaji mzuri ana uwezo mkubwa wa kumiliki mpira na bado kijana, tusubiri kuona,” alisema Tambwe.

Aidha Tambwe alisema anabahati kubwa na klabu ya Yanga hivyo anaamini ataendelea kufanya vizuri zaidi katika safu ya Ushambuliaji ya Yanga.

Tayari Paul Nonga ameshaomba kuondoka klabuni hapo kutokana na kukosa nafasi ya kucheza na kutaka kwenda kujaribu sehemu nyingine.

Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook

Related Posts:

  • HATIMAYE TAMBWE AFUNGUKA UJIO WA CHIRWA YANGAMshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe amesema kucheza timu kubwa kama Yanga kunahitaji ujasiri kutokana na usajili unaofanywa kila wakati. Ujio wa mshambuliaji mpya kwenye kikosi cha Yanga, Mzambia Obrey Chirwa, unaonekana … Read More
  • KIBARUA CHA LAURENT BLANC CHAOTA NYASI PSGKlabu ya PSG imemtimua kocha wake Laurent Blanc, kwa mujibu wa jarida la la L'Equipe la nchini Ufaransa. Taarifa za kutimuliwa kwa kocha huyo bado hazijawa rasmi kwani mpaka hivi sasa klabu ya PSG haijatoa tamko rasmi laki… Read More
  • SIMBA YAITOLEA NJE YANGAKlabu ya Simba imekanusha taarifa zilizotolewa na Ofisa habari wa Yanga Jerry Muro kuwa waliandikiwa barua ya kutaka kutoa ruhusa ya Kessy. Kessy amesajiliwa na Yanga akitokea Simba na amezuiwa kucheza kutokana na mkataba … Read More
  • HII NDO HALI ILIYOPO UWANJA WA TAIFA WATU WAMEFURIKA Kuelekea Mchezo kati ya Yanga na TP Mazembe Leo Jioni Hivi Ndivyo Mashabiki Walivyofurika Uwanja Wa Taifa Mapema Leo Kusubiri Mchezo Huo. KILA LA KHERI YOUNG AFRICA Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa … Read More
  • SIMBA YAPEWA SOMOMwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Ismail Rage ameutaka uongozi wa Simba uliopo madarakani kuacha malumbano na wachezaji. Kumekuwa na kutokuelewana kwa siku za hivi karibuni baina ya wachezaji na viongozi wa Simba kit… Read More

0 comments:

Post a Comment