Thursday, May 12, 2016

MAURICIO POCHETTINO AONGEZA MKATABA SPURS


Kocha wa klabu ya Tottenham Spurs Mauricio Pochettino amesaini mkataba mpya na klabu hiyo utakaomuweka klabuni hapo hadi mwaka 2021. Pochettino alishatangaza wiki 2 nyuma kuwa alishafanya mazungumzo ya awali na klabu hiyo juu ya kuongeza mkataba na sasa hivi ni rasmi kuwa kocha huyo ataendelea kubaki klabuni hapo.

Kocha huyo mwenye miaka 44 alipewa kibarua cha kuinoa klabu hiyo May 2014 na amekuwa na mafanikio makubwa sana katika klabu hiyo, akiiongoza Tottenham kumaliza katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza huku wakiwa wamebakisha mchezo mmoja kumaliza ligi  nafasi ambayo inawahikikishia kushiriki michuano ya UEFA Champions League msimu ujao.

Kocha msaidizi Jesus Perez, na kocha wa makipa Miguel D’Agostino nao pia wamekubali kuongeza mkataba kuendelea kuitumikia klabu hiyo.

Related Posts:

  • MAURICIO POCHETTINO AONGEZA MKATABA SPURS Kocha wa klabu ya Tottenham Spurs Mauricio Pochettino amesaini mkataba mpya na klabu hiyo utakaomuweka klabuni hapo hadi mwaka 2021. Pochettino alishatangaza wiki 2 nyuma kuwa alishafanya mazungumzo ya awali na klabu hiy… Read More
  • HIZI NDO BLA BLA ZA MOURINHO NA MAN U TANGU 2015 Jose Mourinho amekuwa akihusishwa na kujiunga na United tangu Disemba 2015. Jose Mourinho amekuwa akihusishwa na kuchukua mikoba ya Van Gaal United tangu atimuliwe na Chelsea. Soka24 inakuletea mtiririko wa matukio ya… Read More
  • HATIMA YA VAN GAAL MAN UNITED YAWEKWA WAZI Louis Van Gaal amehakikishiwa na mabosi wa United kuwa ataendelea kubaki katika klabu hiyo hadi mwisho wa mkataba wake kwa mujibu wa ripoti ya Daily Star. Mdachi huyo anayeinoa United amekuwa akisemwa sana juu ya uwezo … Read More
  • ARSENE WENGER KUSAINI MKATABA MWINGINE NA ARSENAL Uongozi wa klabu ya Arsenal umepanga kumwongeza mkataba wa miaka 2 kocha wake Arsene Wenger mkataba ambao anatarajiwa kusaini October mwaka huu, lengo likiwa ni kupata muda wa kutosha wa kumtafuta atakaekuwa mrithi wa We… Read More
  • MOURINHO NA VAN GAAL KUFANYA KAZI PAMOJA UNITED Man U wameripoti kwamba wameamua kufanya mabadiliko ya Uongozi wa juu lakini Van Gaal atabaki United. Louis Van Gaal atapewa majukumu ya juu ya utawala katika klabu hiyo ili kumpisha Mourinho kuchukua nafasi hapo Unite… Read More

0 comments:

Post a Comment