Monday, May 16, 2016

KIKOSI CHA SIMBA CHAPEWA LIKIZO FUPI


SIMBA iliyotoka kucheza na Mtibwa Sugar jana na kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila goli lililofungwa na Abdi Banda, imepewa mapumziko mafupi kabla ya kuanza kujiandaa na mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya JKT Ruvu.

Simba kwa sasa wanashika nafasi ya 3 wakiwa wamejikusanyia pointi 62 wakizidiwa pointi moja tu na Azam FC wanaoshika nafasi ya 2 kwa pointi 63, wote wakiwa wamecheza michezo 29.

0 comments:

Post a Comment