Friday, May 27, 2016

ISIKIE KAULI YA MLINDA MLANGO WA YANGA ALLY MUSTAPHA "BARTHEZ" BAADA YA MKATABA WAKE NA KLABU HIYO KUMALIZIKA

Mlinda Mlango wa Yanga Ally Mustapha amemaliza mkataba wake wa kuitumikia klabu ya Dar Young Africans na amesema yupo tayari kuongeza mkataba klabuni hapo endapo maslahi yake yataboreshwa.



Barthez katika misimu minne aliyoitumikia Yanga ameonyesha uwezo mkubwa licha ya mapungufu madogo madogo huku akifanikiwa kushinda Mataji mawili ya ligi kuu, Moja la Shirikisho pamoja na ngao ya hisani.

Ally Mustapha amesema yupo tayari kukaa mezani na Yanga ili kufikia muafaka wa hatima yake klabuni hapo huku akionyesha nia ya kuendelea kubaki klabuni hapo.

"Nimekuwa na mafanikio makubwa hapa Yanga kwa misimu 4 niliyocheza, ambapo ndani yake nimejenga uaminifu kwa makocha wote waliopita na huyu wa sasa lakini pia nimekuwa na marafiki wengi wachezaji na viongozi hivyo sioni sababu ya kuondoka" alisema Barthez alipozungumza na Goal.

Yanga imefanikiwa kutinga katika hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika wakiwa wamepangwa kundi moja na TP Mazembe, MO Bejaia na Medeama, hivyo wanalazimika kukisuka vizuri kikosi chao ili kuleta ushindani katika hatua hii na hatimaye kutinga hatua inayofuata ya nusu fainali.

Related Posts:

  • RASMI:DANI ALVES ATUA JUVENTUSMchezaji wa kimataifa wa Brazil, Dani Alves ametua katika klabu ya Juventus akitokea Barcelona. Dani Alves amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Juventus akitokea Barcelona na kusaini mkataba wa miaka miwili na mabingw… Read More
  • ONYO KALI NA MUHIMU KWA YANGA KUELEKEA MECHI YAO LEOMwenyekiti wa zamani wa Simba Ismail Aden Rage amesema wachezaji wapya waliosajiliwa Yanga hawana leseni za kuichezea timu hiyo katika mchezo wa leo. Rage amesema Sheria ya Usajili ya michuano ya Kombe la shirikisho namba … Read More
  • CHELSEA YATHIBITISHA KUMSAJILI MCHEZAJI HUYU Klabu ya Chelsea imetangaza kumsajili Juan Familia-Castillo akitokea klabu ya Ajax. Kila mwaka Chelsea inawapandisha vijana kutoka katika kikosi chao cha vijana na mwaka huu tayari Castillo amepata bahati hiyo kutokana… Read More
  • MOURINHO AKERWA NA MAAMUZI YA ED WOODWARDKocha mpya wa Man U Jose Mourinho amekerwa na kitendo cha bosi wake Ed Woodward kushindwa kukamilisha dili la Renato Sanches. United tayari imeshakamilisha usajili wa mlinzi kutoka Villarreal, Eric Bailly kwa uhamisho wa p… Read More
  • SIMBA YAITOLEA NJE YANGAKlabu ya Simba imekanusha taarifa zilizotolewa na Ofisa habari wa Yanga Jerry Muro kuwa waliandikiwa barua ya kutaka kutoa ruhusa ya Kessy. Kessy amesajiliwa na Yanga akitokea Simba na amezuiwa kucheza kutokana na mkataba … Read More

0 comments:

Post a Comment