Wednesday, May 25, 2016

HAYA NDO MAAMUZI YA RAFA BENITEZ BAADA YA NEWCASTLE KUSHUKA DARAJA

Kocha wa klabu ya Newcastle United ya Nchini Uingereza ambayo imeshuka daraja rasmi na kwenda kutafuta nafasi ya kurudi ligi kuu katika ligi daraja la kwanza ameweka wazi maamuzi yake kwa klabu hiyo.


Habari kubwa kwa wepenzi na mashabiki wa Newcastle United ni kwamba Kocha Rafa Benitez amekubali kubaki klabuni hapo licha ya timu hiyo kushuka daraja. Benitez tayari ameshasaini mkataba wa miaka mitatu utakaoendelea kumuweka klabuni hapo. Benitez alipewa kibarua cha kuinoa Newcastle United baada ya uongozi wa klabu hiyo kumtupia virago Steve McClaren aliyekuwa kocha mkuu kwa kipindi hicho.



Katika mkataba wake na Newcastle Benitez alikuwa huru kuondoka klabuni hapo endapo klabu hiyo itashuka daraja na kinyume na ilivyotarajiwa na wengi kwamba Benitez angeondoka klabuni hapo mara baada ya Newcastle kuwa imeshuka daraja, yeye mwenyewe ameamua kumwaga wino na kuendelea kubaki.

Related Posts:

  • SIMBA WAZIDI KUWEKA NGUMU KWA YANGA KUHUSU KESSYKlabu ya Simba imesema kama si Yanga kuwapatia fedha hawataandika barua itakayomuidhinisha Hassan Ramadhan Kessy kucheza michuano ya Kombe la shirikisho CAF CC Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Simba, Za… Read More
  • SIMBA YANASA KIFAA KINGINE KIPYAKlabu ya Simba imempa mkataba wa miaka miwili kiungo Mohamed Ibrahimu tayari kwa kuitumikia klabu hiyo msimu ujao. Rais wa Simba ameyathibitisha hayo kwa kusema usajili wa Ibrahimu utasaidia kuimarisha timu yao ambayo ina … Read More
  • MIPANGO YA JULIO KATIKA USAJILIKocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu "Julio" amesema yeye hana mpango wa kusajili wachezaji wa kigeni katika kikosi chake. Julio amesema lengo lake ni kutoa fursa kwa wachezaji wa ndani waweze kuonyesha uwezo wao ili waje ku… Read More
  • FARID MUSSA ASUBIRI RUHUSA YA AZAM FCFarid Mussa ni winga wa Azam FC aliyepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya nchini Hispania na kufanikiwa kufuzu majaribio hayo na sasa anasubiri ruhusa ya klabu tu ili aondoke zake. … Read More
  • SHOMARI KAPOMBE KURUDI MSIMBAZIKlabu ya Simba imesema inapambana kuhakikisha wanamrudisha kikosini beki wao Shomari Kapombe anayeitumikia klabu ya Azam FC kwa sasa. Kapombe ambaye hivi karibuni ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita ligi kuu Vo… Read More

0 comments:

Post a Comment