Monday, May 2, 2016

CHRISTIANO RONALDO FITI 100% KUIVAA MAN CITY



Mshambuliaji hatari wa Real Madrid Christiano Ronaldo yupo fiti kuivaa Manchester City Jumatano hii katika mchezo wa pili wa nusu fainali ya Klabu bingwa Ulaya.
Ronaldo wiki iliyopita alimaliza  mchezo wa kwanza wa nusu fainali bila kufunga goli katika uwanja wa Etihad huku akitoka na maumivu ya mguu, maumivu ambayo yalimuweka nje pia katika mchezo wa La Liga dhidi ya Real Sociedad ambapo Madrid ilishinda kwa goli 1 – 0, hata hivyo kapteni huyo wa timu ya Taifa ya Ureno ameshiriki katika mazoezi ya timu na wachezaji wenzie.

Wakati taarifa za Ronaldo zikionyesha wazi kuwa atauwahi mchezo huo, hali iko tofauti kwa Karim Benzema ambae haijafahamika kama atacheza katika mchezo huo dhidi ya Man City.
Karim Benzema alitolewa wakati wa  mapumziko katika mchezo waliocheza dhidi ya Man City kutokana na kupata maumivu ya misuli.
 



0 comments:

Post a Comment