Sunday, May 22, 2016

BARAZA LA WAZEE WA YANGA WALIA NA GAZETI LINALOMCHAFUA MANJI

Baraza la wazee la klabu ya Yanga hapo jana waliitisha mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya klabu.



Kaika mkutano huo ajenda kubwa ilikuwa ni gazeti linalomwandika vibaya mwenyekiti Yussuf Manji kuelekea uchaguzi mkuu wa klabu, wazee hao wamedai kuwa gazeti hilo linatumiwa na kikundi cha watu wachache wa Yanga ambao hawapendi mafanikio ambayo Manji anaipa Yanga.

Kikundi kinachoshutumiwa kulitumia gazeti hilo ni cha watu ambao walishawahi kuwa viongozi wa Yanga lakini hawakufanikiwa kuwapa Yanga maendeleo makubwa kama inavyoonekana hivi sasa chini ya Uongozi wa Manji.

Wakiongozwa na mzee Ibrahim Akilimali wazee hao waliwapongeza wachezaji wa Yanga,na kumshukuru Yussuf Manji kwa kuijenga Yanga yenye mafanikio na mshikamano huku wakiweka wazi kuwa wao wanamuunga mkono Manji kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Related Posts:

  • VICENT BOSSOU AITWA TIMU YA TAIFA YA TOGO Kocha mpya wa Togo Mfaransa Claude LeRoy amemuita Vicent Bossou katika kikosi cha timu yake ya Taifa .Bossou ameitwa kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha akiwa na klabu ya Yanga. Tayari barua ya mualiko wa kujiu… Read More
  • VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports. Simba w… Read More
  • ACACIA KUSITISHA UDHAMINI NA STAND UNITED KAMPUNI ya ACACIA inayoidhamini timu ya Stand United ya mkoani Shinyanga imesema itaondoa udhamini wake na klabu ya Stand kama Stand itaendeshwa kama kampuni. Taarifa hizo zimekuja mara baada ya Stand kutangaza kuwa kwa … Read More
  • AMIS TAMBWE AMWOMBEA MABAYA KIIZA MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Dar Young Africans Amis Tambwe, amemaliza mchezo wa jana dhidi ya Ndanda FC bila ya kufunga goli, Tambwe anayeongoza katika orodha ya wafungaji bora katika ligi kuu Tanzania bara msim… Read More
  • MBEYA CITY, YANGA KUSIMAMISHA JIJI LEO Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo  utakaowakutanisha Mbeya City ya Jijini Mbeya dhidi ya Yanga ya  jijini Dar-Es-Salaam. Yanga inaingia katika mchezo huu … Read More

0 comments:

Post a Comment