Tuesday, April 12, 2016
Yanga Na Mwadui, Azam FC Na Mtibwa
Michuano ya Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League ( VPL ) inatarajiwa kuendelea tena hapo kesho kwa mechi mbili.
Yanga iliyotoka kumenyana na Al Ahly juzi itawakaribisha vijana wa Jamhuri Kiwelu Julio katika Uwanja wa taifa kesho Jumatano, Mechi nyingine itahusisha timu za Azam Fc na Mtibwa kutoka Jijini Morogoro. Azam Fc watasafiri kuifuata Mtibwa Wakati Yanga wakiwa taifa kuisubiri Mwadui Fc.
Yanga ambayo inashika nafasi ya pili katika Msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 53 ikiwa imeshacheza michezo 22 michezo miwili nyuma ya Simba SC inayoshika nafasi ya kwanza kwa pointi 57 ikiwa imekwishacheza michezo 24, inahitaji Ushindi ili iweze kuchuana na timu za Simba na Azam katika mbio za kumtafuta bingwa wa Ligi kuu Msimu huu.
Azam wao wapo katika nafasi ya 3 wakiwa wamejikusanyia pointi 52 katika michezo 23 waliyocheza.
Mwadui iliyopo chini ya Kocha mwenye maneno mengi Jamhuri Kiwelu Julio inashika nafasi ya 6 ikiwa na pointi 34 katika michezo 25, Mtibwa nao wapo katika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi wakiwa wamekwishacheza Mechi 24 na pointi zao 43.
Mechi hizo ni muhimu kwa timu zote ila ni muhimu zaidi kwa Azam na Yanga ambao wanagombea nafasi ya Ubingwa wa ligi Msimu huu wa 2015/2016.
Related Posts:
AZAM FC YAICHAPA AFRICAN SPORTS Klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati Azam FC ilikuwa ugenini jijini Tanga kupambana na African Sports katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom. Azam FC wamefanikiwa kuibuka na ushindi katika mchezo h… Read More
NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar. Yanga wanaingia katika mc… Read More
YANGA WAKABIDHIWA RASMI KOMBE LAO KLABU Ya Yanga imekabidhiwa kombe lao jioni ya leo katika uwanja wa taifa mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Ndanda FC, mchezo ambao umemalizika kwa sare ya 2 - 2. Ndanda FC ndio walikuwa wa kwanza kupata… Read More
RATIBA YA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO (ASFC) Fainali za kuwania Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) sasa zitafanyika Juni 11, 2016. Mchezo huo wa fainali utakaozikutanisha timu za soka ya Young Africans na Azam… Read More
SIMBA SC WAIDUNGUA MTIBWA SUGAR NYUMBANI KWAO SIMBA ilishuka dimbani hivi leo kucheza na Mtibwa Sugar katika mchezo wao wa 29 wa ligi kuu Tanzania bara,Mchezo uliopigwa mjini Morogoro. Mchezo huo umemalizika kwa Simba SC kushinda kwa goli 1 - 0 goli lililofungwa na… Read More
0 comments:
Post a Comment