Monday, April 18, 2016
TFF Yasikitishwa Na Vurugu Za Mashabiki Wa Simba
Shirkisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limelaani kitendo cha baadhi ya mashabiki wa mpira wa miguu kufanya vurugu mara baada ya mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Toto Africans uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
TFF imesikitishwa na kitendo hicho cha mashabiki wa klabu ya Simba SC, na kusema inalaani kitendo hicho ambacho sio cha kiuana michezo, huku ikiwataka wanachama, washabiki kuheshimu viongozi wa klabu zao waliopo madarakani na kama kuna masuala ya kujadili wakayajadili katika vilabu vyao.
Mashabiki wa klabu ya Simba walifanya vurugu kwa kurusha mawe, wakilenga kuwadhuru viongozi wa klabu hiyo pamoja na wachezaji, magari waliyokuwa nayo baada ya timu yao kupoteza mchezo dhidi ya Toto Africans kwa bao 1- 0.
Jeshi la Polisi baada ya kuwasishi mashabiki kuondoka eneo la uwanja punde tu mchezo ulipomalizika, mashabiki hao walikaidi na kuendelea kurusha mawe hali iliyopelekea jeshi kutumia mabomu ya machozi kuwatanya katika eneo hilo.
Kufutia kitendo hicho, Jeshi la Polisi lilihakikisha bus la timu ya Simba SC na viongozi wake wanaondoka salama uwanjani baada ya kuwatawanya mashabiki hao, kwa kupitia mlango wa karakana ya wachina waliojenga uwanja huo.
Aidha TFF imeviomba vyombo vya Usalama na Ulinzi kuwachukulia hatua kali mashabiki waliohusika na kitendo hicho, kwani kufanya vurugu ni kosa la jinai na wanapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Related Posts:
HABARI ZA MICHEZO MAGAZETINI LEO MEI 20,2016 Soma Vichwa Vya Habari Za Michezo Magazetini Kila Siku Asubuhi Kupitia Hapa Soka24.blogspot.com … Read More
SALUM MAYANGA HUYU NI CLAUDIO RANIERI WA LIGI KUU BARA Kutoka Katika kupigania kutoshuka Daraja Msimu wa 2014/15 Hadi Kushika Nafasi Ya 4 Katika Ligi Kuu Tanzania Bara Msimu Wa 2015/16, Ni Dhahiri kuwa Mayanga Ni Bonge La Kocha. Salum Mayanga Itakumbukwa kuwa msimu wa 201… Read More
MSAFARA WA YANGA WAWASILI SALAMA JIJINI DAR Hapa Timu Ikielekea Makao Makuu Baada Ya kutua katika uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyerere … Read More
MASHABIKI WAFURIKA UWANJA WA NDEGE KUISUBIRI YANGA Msafara wa klabu ya Yanga unatarajia kuwasili Leo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mashabiki wakiwa wanawasubiri kwa hamu kubwa mashujaa wao waliotinga hatua ya robo fainali … Read More
SHABIKI MKUBWA WA YANGA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI Shabiki Mkubwa Wa Yanga Askari Wa Jeshi La Polisi Kikosi Cha Usalama Barabarani Kinyogori Ameuawa Kwa kupigwa Risasi. Kinyogoli Enzi Za Uhai Wake Askari wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajini Kinyogor… Read More
0 comments:
Post a Comment