Sunday, April 24, 2016

Tetesi Za Usajili Barani Ulaya Leo Jumapili April 24, 2016


Barcelona imeandaa Paundi milioni 15 kumnasa Golikipa wa Leicester City
Barcelona inataka kumsainisha mlinda mlango wa Leicester City Kasper Schemeichel kuchukua nafasi ya Marc-Andre ter Stegen. Mabingwa hao wa Ulaya wameandaa kitita cha paundi milioni 15.

Van Gaal Amwekea Vikwazo  Memphis
Kocha wa Man Utd Louis Van Gaal ameweka vikwazo juu ya kumuuza mshambuliaji wake Memphis Depay. Depay ambae ana mwaka mmoja tu tangu ajiunge na klabu hiyo anatakiwa na vilabu vingi vya ulaya.

Tottenham wanaongoza mbio za kumfukuzia Lacazette
Tottenham wanazidi kumfukuzia kwa karibu straika wa Lyon Alexandre Lacazette lakini Manchester United, Everton na Liverpool nao pia wanamuhitaji mchezaji huyo mwenye thamani ya paundi million 23.5

Arsenal na Juve Zamgombea Ibrahimovic Mpya
Arsenal na Juventus wameingia vitani kupigania saini ya kinda anaefananishwa na Zlatan Ibrahimovic kutokana na umbile lake la urefu unaofikia futi 6’3”. Kinda huyo mwenye miaka 16 Dusan Vlahovic anachezea klabu ya Partizan Belgrade.

Related Posts:

  • WEST BROM YAVUNJA REKODI YA KLABU USAJILI WA CHADLI Klabu ya West Bromwich Albion imevunja rekodi ya klabu hiyo kwa kumsajili Winga wa Tottenham Spurs kwa kitita cha Pauni milioni 13. Chadli alijiunga na Spurs akitokea FC Twente kwa uhamisho wa pauni milioni 7 Julai 2013… Read More
  • MAISHA YA FABREGAS CHELSEA YAFIKA UKINGONI Cesc Fabregas ameambiwa na kocha wa klabu ya Chelsea Antonio Conte kuwa anaweza kuondoka klabuni hapo. Conte ametoa kauli hiyo huku kukiwa kumebaki siku 2 tu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya. Kiungo h… Read More
  • AUBAMEYANG AITAMANI REAL MADRID Hakuna ubishi kuwa Nyota wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang anatamani kujiunga na miamba ya soka ya nchini Hispania klabu ya Real Madrid. Aubameyang amewahi kumuahidi babu yake kuwa ipo siku atakuja kucheza k… Read More
  • Rasmi: Wilfred Bony Atua Stoke City Klabu ya Stoke City imekamilisha uhamisho wa Wilfred Bony kwa mkopo akitokea klabu ya Manchester City. Bony aliyefeli kumshawishi kocha mpya wa City, Mhispania Pep Guardiola amefanikiwa kufunga magoli 11 katika michezo 4… Read More
  • Arsenal Yakamilisha Usajili Wa Shkodran Mustafi Klabu ya Arsenal imetangaza rasmi kumsajili beki wa kati wa Valencia Shkodran Mustafi kwa ada ya uhamisho ambayo haijawekwa wazi. Licha ya thamani ya uhamisho wa mchezaji huyo kutowekwa wazi lakini habari za chini chini z… Read More

0 comments:

Post a Comment