Tuesday, April 12, 2016

LIVE Droo Ya Nusu Fainali Kombe La Shirikisho ASFC Leo


Droo ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup), inatarajiwa kufanyika leo Jumanne saa 3 usiku moja kwa moja (live) kupitia kituo cha luninga cha AzamTwo.

Hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho (ASFC) itafanyika live katika kituo cha AzamTwo, ambao kupitia Azamtv ndio wadhamini wa wakuu wa michuano hiyo iliyoibua msisimiko wa mpira wa miguu na kushirikisha timu nyingi zaidi nchini.

Michuano ya Kombe la Shirikisho iliyoanza kwa kushirikisha timu 64 mwishoni mwa mwaka jana, imefikia hatua ya nusu fainali, baada ya Azam FC kuindoa Prisons (3-1), Mwadui FC kuiondosha Geita Gold (3-0) na Yanga SC kuwaondoa Ndanda FC kwa mabao (2-1) na jana Coastal Union Kuwaondoa Simba (1-2).

Mshindi wa Kombe la Shirikisho (ASFC) msimu huu, ataiwakilisha Tanzania mwaka 2017 katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC).

Related Posts:

  • Yaliyosemwa Na TFF Kuhusu Yanga Na Azam Haya Hapa Rais Wa TFF Jamali Malinzi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezitakia kila la kheri klabu za Azam FC na Young Africans ambao ni wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa itayochezwa wikiendi hii. TFF i… Read More
  • Joseph Kimwaga Ajutia Kutua Msimbazi kimwaga Kushoto akishangilia goli Sraika wa Simba, Joseph Kimwaga ametamka kuwa kati ya vitu ambavyo anajutia kwenye maisha yake ya soka, basi ni kutua kuichezea timu hiyo.Mshambuliaji huyo alitua kuichezea Simba kwen… Read More
  • Hizi Ndio Mbinu Zitakazowaua Al Ahly Taifa Kocha Mkuu wa Yanga YANGA inajiandaa kufungasha virago vyao kutoka Kisiwani Pemba ilipoenda kujichimbia kwa siku chache kujiandaa na mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini ikiwa huko Vijana wa Jangwani wamepewa mbin… Read More
  • Kikosi Cha Esperance De Tunis Kutua Nchini Leo Kikosi Cha Esperance De Tunis Azam inatarajia kuvaana na Esperance katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika, mechi ambayo itachezwa kwenye Uwanja wa Chamazi, keshokutwa Jumapili. Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saadi Kawemb… Read More
  • Wadhamini Wa UEFA Kuboresha Soka La Tanzania Shirikishio la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru kampuni ya bia ya Heineken ambao ni wadhamini wakuu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya (UEFA) kwa kujitolea kufanya ukarabati wa viwanja vitatu vya mpira w… Read More

0 comments:

Post a Comment