Sunday, February 26, 2017

Atletico Madrid 1 - 2 Barcelona, messi aipeleka Barcelona kileleni


Timu ya Barcelona imetambatia timu ya Atletico Madrid baada ya kuichapa goli 2 - 1.
Mpira ulianza kwa kasi kila timu ikifika langoni mwa mpinzani, 4' Diego Godin alikosa goli la wazi.

mpira uliendelea kuwa wa kosa ni kukose mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika kila timu ilikwenda vyumbani na kuacha ubao ukisomeka 0 - 0.

kipindi cha pili kilianza kwa mashambulizi ya nguvu kwa kila timu na mnamo 48' Luis Suarez alikosa goli la wazi baada ya kupenyezewa pasi na Neymar.

51' gezma alipiga shuti kali lakini umakini wa kipa aliweza kuokoa mpira huo. 64' rafinah anaipatia barca bao baada ya piga nikuge langoni mwa Atletico Madrid.

dakika ya 70 Atletico walipata faulo karibu na eneo la kumi na nane na ilipigwa kiufundi na kutua kwenye kichwa cha Diego Godin na kuipatia timu yake goli pekee kwa siku ya leo.

75' Angel Correa alimfanyia rafu mbaya Jeremy Mathieu na kupewa kadi ya njano.
77' Jeremy Mathieu anatoka nje anaingia Lucas Digne baada ya kushindwa kuendelea na mchezo huo.

mabadiliko ya kumuingizaAndre Gomes kuchukua nafasi ya Sergi Roberto 85' yaliongeza mashambulizi na 86' messi anaipatia Barcelona goli la pili baada ya kumalizia kazi aliyoifanya yeye mwenyewe na kumgonga beki wa Atletico Madrid kabla ya kuumalizia mpira huoo.

mpaka mpira unamalizika Atletico Madrid 1 - 2 Barcelona.
kwa matokeo hayo Atletico wanasalia na pointi zao 45 baada ya mechi 24 katika nafasi ya 4.

Barcelona wamekwea mpaka kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya michezo 24 wamejikusanyia pointi 54



0 comments:

Post a Comment