Thursday, January 26, 2017

Rufaa ya polisi Dar es Salaam dhidi ya mchezaji wa simba Novalty Lufunga kucheza huku akiwa na kadi nyekundu yagonga mwamba


Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania limeitupilia mbali rufaa ya timu ya polisi Dar es salaam waliokata kutaka wapewe ushindi katika mchezo wao wa raundi ya tano  ambao simba ilishinda kwa 2 -0,

Mchezaji Novalty Lufunga aliekatiwa rufaa alipata kadi nyekundu katika mchezo wa mwisho kwa simba wa  Azam Sports Federation Cup 2015/2016 ambapo simba ililala katika mchezo huo wa 11april 2016 kuondoshwa mashindanoni.

Kanuni za  Azam Sports Federation Cup zinaweka wazi kuwa kadi ya njano au nyekundu inaisha pale tu mashindano husika yanapoisha labda itokee kadi hiyo imeongezewa na adhabu nyingine, kama itakuwa imeongezewa adhabu basi klabu na mchezaji watataarifiwa  kwa maandishi.

Hivyo basi kwa kanuni hiyo ya mashindano polisi Dar itakuwa imetupwa nje rasmi katika mashindano hao ya Azam Sports Federation Cup

0 comments:

Post a Comment