Saturday, January 28, 2017

Liverpool 1 - 2 Wolverhampton Wanderers


mchezo wa mapema wa kombe la FA umemalizika kwa matokeo ambayo liverpool watayakumbuka sana.
Ikiwa ndani ya dimba la anfield majogoo wa jiji wamekubali kipigo cha magoli 2 – 1 kutoka kwa Wolverhampton Wanderers .
Iliwachukua dakika moja tu baada ya kuanza kwa mchezo kwa Wolverhampton Wanderers  kujipatia goli la kuongoza kupitia kwa Richard Stearman.

Mchezo uliendelea kuwa  wa vuta ni kuvute na ukishuhudia kadi nne za njano tatu kwa wageni  Wolverhampton Wanderers na moja kwa Liverpool.

Liverpool wakiwa wanatafakari kuchomoa goli hilo moja mnamo dakika ya 41 Andreas Weimann aliongeza maumivu kwa goli zuri na kuipa timu yake uongozi wa goli 2 – 0 mpka mapumziko.
Kipindi cha pili kila timu ilifanya mabadiliko kwa upande wa Liverpool waliwatoa Connor Randal 46’ nafasi yake kuchukuliwa na Philippe Coutinho, wakamtoa tena Roberto Firmino 65’ nafasi yake kuchukuliwa na Daniel Sturridge, na walihitimisha kwa kumtoa Ovie Ejaria 74, na kumuingiza Emre Can.
Kwa upande wa Wolverhampton Wanderers wao pia walifanya mabadiliko matatu kwa kuwatoa Helder Costa 67’ na kuingia Connor Ronan, ilimtoa tena Nouha Dicko 70’ nakuingia Jon Dadi Boedvarsson, ilihitimisha kwa kumtoa  Andreas Weimann 77’ na kuingia Joe Mason.

Mabadiliko hayo yaliisadia Liverpool kupata goli la kufutia machozi mnamo dakika ya 86 kupitia Orig


FT Liverpool 1 – 2 Wolverhampton Wanderers

0 comments:

Post a Comment