Thursday, January 26, 2017

Huyu Ndiye Anayekimbiza Kwa Magoli AFCON 2017

Anaitwa Junior Kabananga Mchezaji wa Congo DR.

Katika Michuano inayoendelea huko nchini Gabon kwa sasa, mchezaji nyota wa timu ya taifa ya Congo DR, Kabananga ndiye anayeongoza katika orodha ya wafungaji katika michuano hiyo.

Kabananga amefanikiwa kutupia nyavuni magoli matatu, magoli ambayo amefanikiwa kuyapata katika mechi zote tatu alizocheza, akifunga goli moja kila mechi na kuisaidia timu yake kutinga hatua ya robo fainali ya AFCON 2017.

Congo DR itacheza dhidi ya timu ya taifa ya Ghana katika hatua ya robo fainali wikiendi hii.

0 comments:

Post a Comment