Sunday, January 29, 2017

Bossou Kucheza Dhidi Ya Mwadui Leo Taifa?

Beki kisiki wa Yanga, Vicent Bossou anatarajia kurejea nchini Leo Jumapili akitokea nchini kwao Togo baada ya kukosekana kwa muda wa mwezi mmoja alipokuwa akiitumikia timu yake ya taifa huko nchini Gabon katika michuano ya AFCON.

Baraka Deusdedit amesema Bossou amewahakikishia Yanga kuwa Jumapili hii atakuwa amewasili kambini tayari kwa kuitumikia klabu yake ya Dar Young Africans.

“Tumeongea na mchezaji na ametuhakikishia hadi Jumapili atakuwa aewasili kambini kwasababu timu inamuhitaji kutokana na mikakati tuliyokuwa hivyo tunamuombea mungu ili aweze kurejea salama,”amesema Baraka.

Togo, imeondolewa katika michuano hiyo ya Mataifa ya Afrika katika hatua ya makundi baada ya kuambulia pointi moja tu katika mechi zao tatu walizocheza katika hatua ya makundi, ilichapwa 3-1 na Congo DR, ikaja kuchapwa tena 3-1 dhidi ya Morocco kabla hawajatoa suluhu dhidi ya Ivory Coast.

Related Posts:

  • Mnyama Afanyiwa Ujangili TaifaTimu ya soka ya Simba SC imejikuta nje ya michuano ya FA baada ya kupokea kichapo toka kwa timu ya Coastal Union. Katika mchezo huo wa vuta nikuvute Coasta ilikuwa yakwanza kutikisa nyavu za Simba baada ya mchezaji Yusuf kupi… Read More
  • Joseph Kimwaga Ajutia Kutua Msimbazi kimwaga Kushoto akishangilia goli Sraika wa Simba, Joseph Kimwaga ametamka kuwa kati ya vitu ambavyo anajutia kwenye maisha yake ya soka, basi ni kutua kuichezea timu hiyo.Mshambuliaji huyo alitua kuichezea Simba kwen… Read More
  • "Sisi Mashabiki Wa Yanga Timu Hatuielewi Kwa Sasa" Mashabiki wa Yanga wameshindwa kuvumilia kinachoendelea kwa sasa katika timu yao hali iliyochangiwa pia na sare ya Juzi dhidi ya Al Ahly. Hali hiyo imepelekea Mashabiki hao kumfuata Kocha Charles Boniface Mkwasa anaeitumik… Read More
  • Yanga Na Mwadui, Azam FC Na Mtibwa Michuano ya Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League ( VPL ) inatarajiwa kuendelea tena hapo kesho kwa mechi mbili. Yanga iliyotoka kumenyana na Al Ahly juzi itawakaribisha vijana wa Jamhuri Kiwelu Julio … Read More
  • Kombe La FA Ngoma nzito.... Angalia matokeo ya droo hapa.Droo ya michuano ya Kombe la Shirikisho hatua ya nusu fainali, leo imepangwa. Mwadui FC imepangiwa Azam FC na mechi ya kwanza itachezwa mjini Shinyanga wakati Yanga wao watacheza na Coastal Union ambao wataanzia mjini Tanga. … Read More

0 comments:

Post a Comment