Friday, December 2, 2016

barcelona vs Real madrid ni EL CLASICO ya kihistoria




Ubishi kumalizwa Camp Nou siku ya jumamosi wakati miamba miwili ya soka Barcelona na Real Madrid watakapoonyesha kazi katika mchezo muhimu wa ligi kuu ya nchini Hispania maarufu kama ‘LaLiga Santander’

Tukiiangalia Barcelona, kwa msimu huu ni kama mambo yanawaendea vibaya hawawapi raha mashabiki wao kama walivyozoea, kiufundi baada ya beki wao kisiki Gerard Pique Kuwa na maumivu ya ankle na kucheza chini ya kiwango kwa muagentina Javier Mascherano huenda kukamlazimu kocha Luis Enrique kocha wa Barcelona kumuanzisha Samuel Umtiti ambae katoka kwenye majeruhi.  Chakufurahisha kwa Barcelona ni kupona kwa Iniesta na Alba hivyo kutaongeza morali kwa wachezaji.

Kwa upande mwingine kocha zidane atakuwa katika wakati mgumu pale atakapowakosa wachezaji wake muhimu wa kikosi cha kwanza Toni Kroos na Gareth Bale hivyo ambapo inatabiriwa huenda akabadili mfumo wa uchezaji kutoka 4 -3 -3 kwenda 4 -2 -3 -1 akiwatumia Casemiro , Mateo Kovacic na Luka Modric eneo la katikati.

Zidane alipohojiwa na vyombo vya habari alisema yeye anasubiri dakika 90 wakati
Takwimu kwa timu zote mbili kuelekea mchezo huo zinaibeba real Madrid kuibuka na ushindi na kukaribia kuikuta rekodi ya 1988/89 ya kucheza michezo 34 bila kupoteza mpka sasa Madrid imecheza michezo 31 bila kupoteza


Nani kuibuka mbabe tusubiri dakika 90 katika dimba la nou camp kesho jumamosi kuanzia saa 18:15


Kombe            Real Madrid vs                                    matokeo 
Copa                  Cultural L.                                             6-1      home
laLiga               Sporting Gijon                                         2-1     home
Champions         Sporting Portugal                                    1-2    away
laLiga               Atlético-madrid                                         0-3     away
laLiga                Leganés                                                   3-0  home

kombe                           Barcelona vs                               matokeo
Copa                     Hércules                                                 1-1    away
Liga                       R. Sociedad                                            1-1   away
Champions         Celtic Glasgow                                            0-2   away
Liga                      Málaga                                                     0-0   home

Liga                     Sevilla                                                       1-2  home



michezo mingine ya laliga kesho decemba 3 ni kama ifuatavyo:
Granada vs Sevilla               15:00
Leganes vs Villarreal           20:30
Atletico Madrid vs Espanyol   22:45

0 comments:

Post a Comment