Saturday, October 15, 2016

MATOKEO YA MICHEZO YA EPL LEO JUMAMOSI


Ligi kuu ya uingereza imeendelea tena leo kwa michezo sita kupigwa katika viwanja sita tofauti
Mchezo wa mapema ulipigwa Stamford bridge pale Chelsea walipoiadhibu bila huruma bingwa mtetezi wa ligi hiyo Leicester City kwa goli 3 bila majibu kwa  magoli ya Diego costa dakika ya 7 kabla ya Eden Harzad kufunga la pili dakika ya 33 na msumari wa mwisho ulipigiliwa na mnigeria Victor Mosses dakika ya 80 na kuifanya Chelsea kufikisha alama 16 na kupanda mpaka nafasi ya 5
Wakati huohuo mambo yanaendelea kumuendea kombo Gudiola baada ya leo kukaliwa kooni na kulazimishwa kutoka sare ya goli 1 kwa 1 na Everton, ilikua ni Everton ndio walioanza kulifumania lango la Man city dk 64 kupitia kwa Lukaku kabla ya Nolito kuisawazishia city katika dk 72
Stoke city wao walitoa onyo kwa sunderland kwa kuibugiza magoli miwili kwa bila kwa magoli ya Joe Allen dk 9 na 45 ya mchezo
Arsenal wameendelea kutoa dozi na kuikaribia man city kileleni baada ya kuipiga kumbo Swansea city 3 2 kwa magoli miwili ya Theo Walcot na moja la Mesut Ozil magoli ya Swansea yalifungwa na Sigurdsson na Borjan Boston
AFC Bournemouth imefanya kufuru  kwa Hully City baada ya kupiga goli 6 kwa  1

West Bromwich Albion wameondoa furaha ya Tottenham Hotspur waliyokua nayo wiki moja iliyopita baada ya kuifunga man city baada ya kugawana alama mojamoja Kutokana na sare ya 1 1 goli la Tottenham Hotspur likifungwa na Dele Alli dk 89 huku lile la mapema la West Bromwich Albion likifungwa dk44 James mc Clean


Related Posts:

  • Tetesi Mpya Za Usajili Arsenal Ungana na Soka24, kwa habari za papo kwa papo za usajili katika klabu kubwa na pendwa zaidi duniani, hapa nimekuwekea yanayojiri katika klabu ya Arsenal hivi sasa. Arsenal katika mbio za Kumuwania Mbappe klabu ya Arsenal… Read More
  • PSG Wakubali Yaishe Kwa Aubameyang Vigogo wa soka nchini Ufaransa, PSG wamekubali kutoa paundi milioni 61 kuinasa saini ya mshambuliaji wa Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Licha ya gharama hizo za uhamisho PSG pia wamekubali kumlipa nyota huyo kutoka b… Read More
  • Griezmann Kubaki Atletico Madrid Mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann amedokeza kwamba huenda asiihame klabu yake, licha ya kuwindwa na klabu  kubwa Ulaya ikiwemo Manchester United. Mfaransa huyo wa miaka 26 aliandika kwenye Twitter: "… Read More
  • Ozil, Sanchez Washusha Presha Ya Mashabiki Arsenal Washambuliaji machachari wa klabu ya Arsenal Mesut Ozil na Alexis Sanchez wameshusha presha ya mashabiki wengi wa Arsenal baada ya uvumi kuenea kuwa nyota hao wataihama klabu hiyo. Taarifa za hivi punde zinadai kuwa wach… Read More
  • Tetesi Mpya Za Usajili Manchester United Tetesi za usajili katika klabu ya Manchester United. Man United Kukamilisha Uhamisho Wa Lacazette klabu ya Manchester United ipo mbioni kuhakikisha inamsajili straika wa Lyon Alexandre Lacazette, kwa mujibu wa L'Equipe … Read More

0 comments:

Post a Comment