Kocha Wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini Uingereza Leicester City, Claudio Ranieri ameionya Man United kuwa wasitegemee mchezo rahisi leo.
Ranieri amedai anaamini kuna kitu kizuri kinakuja katika klabu yake kuelekea mchezo wao leo dhidi ya Mashetani wekundu nchini ya kocha Mourinho mchezo wa ngao ya Jamii.
"Nafanya kazi katika ari ileile, kujiamini kulekule na mtazamo uleule" alisema Ranieri.
"Hakuna kilichopungua, ni jukumu langu kuhakikisha wachezaji wangu wanakuwa na njaa ileile ya mafanikio" Aliongeza Mreno huyo aliyeipa ubingwa wa kihistoria Leicester.
Ranieri bado anaendelea kuwa na imani kubwa na kikosi chake na anajua wazi kuwa anapaswa Leicester kucheza katika ari ileile iliyopelekea kutwaa ubingwa wa EPL msimu wa 2015/16.
"Uimara wetu si katika kumiliki mpira, ni kucheza vile tunavyotaka cha msingi ni kuwa fiti asilimia 100, hivyo haitakuwa kazi rahisi kwa Manchester United leo ndani ya dakika 90".
Sunday, August 7, 2016
CLAUDIO RANIERI AIONYA MAN UNITED
Related Posts:
HUU NDIO USAJILI WA KWANZA WA MOURINHO MAN UTD MANCHESTER United wamekubali kulipa ada ya uhamisho ya Euro Milion 80 ili kumnasa nyota wa Benifica Renato Sanches. Gazeti la Michezo la Ureno limeripoti kuwa katika dili hilo Man Utd watalazimika kulipa Euro Milioni 40 … Read More
SIMON MIGNOLET HATARINI KUTIMULIWA LIVERPOOL Mlinda mlango wa Liverpool Simon Mignolet ameonekana kuwaangusha mamilioni ya mashabiki wa Liverpool msimu huu na kocha Klopp anafikiria kumleta kipa mwingine anayechezea Barcelona kwa sasa Marc-Andre ter Stegen. … Read More
MEMPHIS DEPAY AFUTA PICHA ZOTE ZA MAN UTD INSTAGRAM Wakati akihusihusishwa na tetesi za kuondoka klabuni hapo Mephis Depay amefuta picha zake zote instagram, kitu ambacho ni kama ishara tosha kuwa Mdachi huyo yupo mbioni kutimka klabuni hapo akiwa ameitumikia klab… Read More
ANTONIO CONTE AKUBALI KUMUUZA STAA HUYU KWA PAUNDI ML. 50 KOCHA mpya wa Chelsea Antonio Conte licha ya kuwa anapenda kuwaacha mastaa wake wote katika kikosi hicho na alishaitisha kikao na timu kuliweka wazi suala hilo, amekubali kuwa licha ya kukosa nafasi ya kucheza klabu bing… Read More
LOUIS VAN GAAL ANAAMINI BADO ANA NAFASI YA KUBAKI MAN UTD Louis Van Gaal bado anaamini anaweza akatetea kibarua chake kwa kushinda kombe la FA na kumaliza katika nafasi ya Nne katika msimamo wa ligi kuu nchini England-EPL. Matumaini ya Mdachi huyo kumaliza mkataba … Read More
0 comments:
Post a Comment