Saturday, July 9, 2016

NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA

Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu mbalimbali.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amewataja wachezaji hao kuwa ni Mwinyi Haji na Geofrey Mwashiuya wanaosumbuliwa na maumivu ya goti wakati Deus Kaseke yeye anauguza majeraha aliyoyapata baada ya kupata ajali ya pikipiki.

"Tuna majeruhi watatu hadi sasa wanaendelea kupatiwa matibabu,bado hawajaanza mazoezi yoyote, lakini wachezaji wengine wote wanaendelea na mazoezi vizuri" alisema.

Aidha Mchezaji Juma Mahadhi ambaye aliumia katika mchezo dhidi ya TP Mazembe amepona na tayari anaendelea na mazoezi na wachezaji wenzake kujiandaa na mchezo huo dhidi ya Medeam FC.
Chirwa ambaye alikwenda nchini kwao kwa ajili ya mchezo dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia Congo amesharejea na yupo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

Yanga imekwishacheza mechi mbili katika hatua hiyo ya makundi na wamepoteza katika michezo yote miwili na kushika nafasi ya mwisho katika msimamo wa kundi A, huku TP Mazembe akiwa kinara wa kundi hilo kwa kujikusanyia alama 6 katika michezo yote miwili aliyocheza.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook



Related Posts:

  • RUVU SHOOTING KUKIPA NGUVU KIKOSI CHAORuvu Shooting ipo katika mipango ya kusajili wachezaji saba ili kujiimarisha kabla hawajaanza kipute cha ligi kuu Vodacom msimu wa 2016/17. kwa sasa Ruvu Shooting inaendelea na kambi kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwa… Read More
  • KAPOMBE ATOA SHUKRANI ZAKE KWA MASHABIKIBAADA ya kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa mashabiki msimu uliopita, beki wa kulia wa Azam FC, Shomari Kapombe, amewashukuru mashabiki kwa kuonesha imani naye na kumfanya awe mshindi wa tuzo hiyo. Pia, ameeleza masikitiko ya… Read More
  • CHIRWA ATUA JANGWANI KWA SH. MILIONI 240Mshambuliaji raia wa Zambia, Obrey Chirwa amejiunga na Yanga kwa dau la sh. Milioni 240 akitokea katika klabu ya FC Platinum za Zimbabwe. Chirwa ameifungia Platinum mabao matano katika mechi nane alizocheza kwenye ligi kuu… Read More
  • KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBAHarakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo. Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti … Read More
  • CAF YAISAFISHIA NJIA YANGAShirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF), limemthibitisha beki Hassan Kessy kuichezea Yanga katika michuano ya Kombe la CAF CC katika hatua ya makundi. Caf pia imetuma leseni ya wachezaji wengine watatu wa Yanga walioonge… Read More

1 comments:

  1. Kazi nzuri endeleeni kuwajuza wananchi yanayoendelea kujiri.

    ReplyDelete