Saturday, July 9, 2016

NYOTA WATATU YANGA KUKOSA MCHEZO DHIDI YA MEDEAMA

Klabu ya Yanga inaendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho Barani Afrika hatua ya makundi dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana lakini huenda wachezaji wake watatu wakaukosa mchezo huo kutokana na sababu mbalimbali.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amewataja wachezaji hao kuwa ni Mwinyi Haji na Geofrey Mwashiuya wanaosumbuliwa na maumivu ya goti wakati Deus Kaseke yeye anauguza majeraha aliyoyapata baada ya kupata ajali ya pikipiki.

"Tuna majeruhi watatu hadi sasa wanaendelea kupatiwa matibabu,bado hawajaanza mazoezi yoyote, lakini wachezaji wengine wote wanaendelea na mazoezi vizuri" alisema.

Aidha Mchezaji Juma Mahadhi ambaye aliumia katika mchezo dhidi ya TP Mazembe amepona na tayari anaendelea na mazoezi na wachezaji wenzake kujiandaa na mchezo huo dhidi ya Medeam FC.
Chirwa ambaye alikwenda nchini kwao kwa ajili ya mchezo dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia Congo amesharejea na yupo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

Yanga imekwishacheza mechi mbili katika hatua hiyo ya makundi na wamepoteza katika michezo yote miwili na kushika nafasi ya mwisho katika msimamo wa kundi A, huku TP Mazembe akiwa kinara wa kundi hilo kwa kujikusanyia alama 6 katika michezo yote miwili aliyocheza.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook



Related Posts:

  • WALICHOKIFANYA MO BEJAIA KUHAKIKISHA YANGA HAWATOKI ALGERIA Wapinzani wa Yanga katika Kundi A la michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, MO Bejaia kutoka Algeria wamefanya mabadiliko katika benchi lao la ufundi. Kocha Nacer Sandzak ameteuliwa kuwa kocha mkuu mpya kuchukua … Read More
  • YANGA KUANZA KAMBI RASMI LEO Timu ya Dar Young Africans inatarajiwa kuingia kambini leo kujiandaa na michezo ya hatua ya makundi CAF Confederation Cup. Yanga itacheza mchezo wake wa kwanza katika hatua hiyo Juni 19 dhidi ya MO Bejaia ya nchini Algeri… Read More
  • KOCHA YANGA ATOA ONYO KALI CAFKocha Mkuu wa Yanga, Hans Van Pluijm ameliomba shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) kuchukua hatua kali kwa klabu ambazo mashabiki wake wataleta vurugu dhidi ya timu pinzani. Pluijm ametoa onyo hilo kwa CAF wakati huu… Read More
  • CAF YAISAFISHIA NJIA YANGAShirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF), limemthibitisha beki Hassan Kessy kuichezea Yanga katika michuano ya Kombe la CAF CC katika hatua ya makundi. Caf pia imetuma leseni ya wachezaji wengine watatu wa Yanga walioonge… Read More
  • MEDEAMA SC KUJITOA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA (CAF CC)Medeama huenda ikajitoa katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, kutokana na hali ngumu ya kifedha. Medeama imepangwa kucheza na TP-Mazembe katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo Juni 19,2016. CAF bado h… Read More

1 comments:

  1. Kazi nzuri endeleeni kuwajuza wananchi yanayoendelea kujiri.

    ReplyDelete