Wednesday, June 1, 2016

UNAKUMBUKA KIFO CHA SHABIKI WA YANGA SAJINI KINYOGORI? HUYU KAKIKRI KUHUSIKA MOJA KWA MOJA

Wiki chache zilizopita soka24 iliripoti juu ya kifo cha Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani Sajini kinyogori, Taarifa za uchunguzi zimebaini kuwa mkewe amehusika na mauaji hayo.


Sajini Kinyogori aliuawa kwa kupigwa risasi nyumbani kwao eneo la Mwadenge, Mkoani Pwani, Wauaji wa Askari huyo hawakuweza kubainika mara moja, lakin ripoti za hivi karibuni kutoka kwa kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar Es Salaam Simon Siro zinasema kwamba, Mke wa Askari huyo ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi, amekiri kuhusika na mauaji hayo ya mumewe.


Mwanamke huyo amesema alihusika katika njama za kumuua mumewe kwa kile alichodai kuwa Askari huyo alimuacha na kwenda kuoa mwanamke mwingine.
Kamanda Siro amesema Mwanamke huyo yupo chini ya ulinzi wa Askari Polisi pamoja na watuhumiwa wengine wakichukuliwa maelezo.

0 comments:

Post a Comment