Tuesday, May 10, 2016

MBEYA CITY, YANGA KUSIMAMISHA JIJI LEO


Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo  utakaowakutanisha Mbeya City ya Jijini Mbeya dhidi ya Yanga ya  jijini Dar-Es-Salaam. Yanga inaingia katika mchezo huu  ikiwa tayari imeshajihakikishia ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2015/16 baada ya Simba kupoteza mchezo wake dhidi ya Mwadui FC,mechi hiyo  inatarajiwa kuwa kali na ya kuvutia licha ya Yanga kuwa mabingwa tayari kutokana na ushindani uliopo baina ya timu hizi, Mbeya City inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kujihakikishia kubaki kwao katika ligi kuu msimu ujao.

0 comments:

Post a Comment