Tuesday, April 12, 2016

"Mapema Sana Kumwita Van Gaal Failure" Jordi Cruyff

Van Gaal

Nyota wa Zamani wa Barcelona na Manchester United Jord Cruyff amewabeza wanaomponda kocha wa Manchester United Louis Van Gaal kwa kuwaambia ni mapema sana kumwona kocha huyo ni failure (aliefeli ). Jord aliongea maneno hayo yanayoonyesha kumkingia kifua Louis Van Gaal anaeonekana kuwa si chochote mbele ya Mashabiki kutokana na mwenendo wa timu hiyo kwa sasa.

“Louis Van Gaal anahitaji kupewa muda zaidi Man United”  yalikuwa ni maneno ya Jordi Cruyff.
Tetesi za kocha wa zamani wa Chelsea Jose Mourihno kujiunga na Man United kuchukua nafasi ya Van Gaal Msimu wa 2016/2017 Cruyff anaona sio kitu sahihi kwa sasa
.
Jordi Cruyff Nyota Wa Zamani Wa Man U
“Nafikiri neno kufeli linamaana kubwa sana” alisema Jordi akiiambia Omnisport machi 18 mwaka huu. “kuna mechi nyingi bado za kucheza, kama wakiishia kushinda kombe la FA na kumaliza katika nafasi ya pili katika ligi sidhani kama watu wataona huko ni kufeli, wataona hiyo ni kama kujiimarisha” aliongeza Cruyff.

“Itakuwa ni kitendo cha kikatili na cha haraka sana kumfukuza kwa sasa, japo ni wazi kuwa mambo hayaendi  sawa kama ambavyo wengi walitarajia licha ya uwekezaji mkubwa uliofanyika klabuni hapo” alisema Cruyff.


Man United ipo katika kipindi kigumu kwa sasa kufuatia vichapo inavyopokea kutoka kwa timu pinzani pia ikiwa haina uhakika wa kushiriki michuano ya UEFA msimu ujao. Mchezo wao wa mwisho waliocheza na Tottenham walikubali kichapo cha magoli matatu kwa bila na Wanatarajia kucheza na West Ham United Jumatano hii katika Uwanja wa Upton Park.

Related Posts:

  • USIPITWE NA HAYA MAMBO MUHIMU USAJILI LIGI KUU UINGEREZA 2016-17 Klabu za Ligi ya Premia zilitumia zaidi ya £155m siku ya mwisho ya kuhama kwa wachezaji kipindi cha majira ya joto na kufikisha jumla ya pesa zilizotumiwa hadi rekodi mpya ya £1.165bn. Klabu zilikuwa tayari zimetumia j… Read More
  • GARETH BALE HAJALI KUFUNIKWA NA POGBA Mchezaji wa Real Madrid Gareth Bale anasema kuwa hashtushwi na hatua ya kupoteza taji la kuwa mchezaji ghali zaidi duniani alilopoteza kwa Paul Pogba. Bale alipoteza taji hilo kwa Pogba baada ya miaka mitatu kufuatia hatu… Read More
  • Fifa Yaleta Waraka Mpya Wa Usajili Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), limesambaza waraka mpya kwa wanachama wake, likiwamo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ukisema mameneja wote wa usajili wa wachezaji kwa mfumo wa Mtandao (TMS-Trans… Read More
  • YAYA TOURE ATUPWA NJE YA KIKOSI CHA MAN CITY Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amemwacha nje kiungo wa kati wa timu hiyo yaya Toure katika kikosi chake cha kombe la vilabu bingwa Ulaya mwaka 2016-17. City haikuweza kuweka zaidi ya wachezaji 17 wa kigeni katika kik… Read More
  • ALAVES YASHUSHA KIMBUNGA CAMP NOU Klabu ya Barcelona imepokea kichapo kutoka kwa timu ya Alaves Jana Jumamosi cha magoli 2-1. Goli la Mathieu dakika ya 46 na lile la Ibai Gomez dakika ya 63 yalikamilisha ushindi huo walioupata katika dimba la Camp Nou, hu… Read More

0 comments:

Post a Comment