Sunday, April 24, 2016

Azam FC Yatinga Fainali Kombe La FA


Azam Fc imetinga hatua ya fainali ya kombe la shirikisho baada  ya kuiondosha Mwadui Fc kwa mikwaju ya penati 5-3. Mechi hiyo ambayo ilikuwa na kasi na ushindani mkubwa ilimalizika kwa sare ya 1 - 1 katika dakika 90 za kawaida, katika dakika 30 za nyongeza Azam Fc walifanikiwa kupata goli la pili dakika ya 96 kupitia kwa Bocco.
Mwadui walisawazisha goli hilo dakika ya 120 kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa azam kunawa katika eneo la penati box.
Hata hivyo Mchezaji mmoja wa Mwadui alipoteza penati moja Huku Azam wao wakifunga penati zote Tano.
Azam FC sasa hivi wanasubiri hatima ya mechi kati ya Coastal Union na Yanga SC iliyovunjika kutokana na vurugu zilizosababishwa na mashabiki wa Coastal Union ili wajue nani wanacheza nae katika hatua ya fainali.






pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • KIMESHAELEWEKA YANGA WAPYA WOTE RUKSA ISIPOKUWA HUYUWachezaji wote wapya wa Yanga wamethibitishwa kuwa huru kuanza kuitumikia klabu hiyo isipokuwa Hassan Ramadhan Kessy. Yanga imewasajili wachezaji watano hadi sasa ambao ni Andrew Vicent, Juma Mahadhi, Ben Kakolanya, Hassan… Read More
  • MIPANGO YA JULIO KATIKA USAJILIKocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kiwelu "Julio" amesema yeye hana mpango wa kusajili wachezaji wa kigeni katika kikosi chake. Julio amesema lengo lake ni kutoa fursa kwa wachezaji wa ndani waweze kuonyesha uwezo wao ili waje ku… Read More
  • SIMBA WAZIDI KUWEKA NGUMU KWA YANGA KUHUSU KESSYKlabu ya Simba imesema kama si Yanga kuwapatia fedha hawataandika barua itakayomuidhinisha Hassan Ramadhan Kessy kucheza michuano ya Kombe la shirikisho CAF CC Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Simba, Za… Read More
  • KIWANGO KIBOVU CHA HAJI MWINYI CHAMUUMIZA PLUIJMKiwango cha beki wa kushoto wa Yanga Haji Mwinyi kinaonekana kushuka hali inayomfanya kocha Hans Pluijm kutafuta namna ya kulifanyia kazi suala hilo. Haji Mwinyi ni beki mwenye kipaji kikubwa anayeweza kuimudu vizuri nafas… Read More
  • SHOMARI KAPOMBE KURUDI MSIMBAZIKlabu ya Simba imesema inapambana kuhakikisha wanamrudisha kikosini beki wao Shomari Kapombe anayeitumikia klabu ya Azam FC kwa sasa. Kapombe ambaye hivi karibuni ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita ligi kuu Vo… Read More

0 comments:

Post a Comment