Kepteni wa timu ya taifa ya Tanzania anaekipiga katika timu ya Genk Mbwana Samatta ameendelea kuwa mwiba katika safu ya ulinzi anaowekewa na timu pinzani Barani ulaya.
Jana usiku Samatta alifunga mara 2 na kuisaidia timu yake ya Genk kupata ushindi ugenini wa 5 – 2 dhidi ya Gent zote za Ubeligiji.
Samatta ambae kwasasa yupo katika kiwango bora kabisa alipata magoli hayo dakika ya 41 na 72.
Magoli mengine ya Genk yalifungwa na Ruslan Malinovsky 21’, Omar Colley 33’ na Jere Uronen 45’
Magoli ya Gent yalifungwa na Samuel Kalu 27’ na Kalifa Coulibaly 61’
Matokeo mengine jana ni kama ifuatavyo:-
Celta de Vigo 2-1 FK Krasnodar
APOEL Nicosia 0-1 Anderlecht
FC Schalke 04 1-1 Borussia Mönchengladbach
Olympique Lyon 4-2 AS Roma
FK Rostov 1-1 Manchester United
Olympiakos Piraeus 1-1Besiktas
FC Kopenhagen 2-1 Ajax
0 comments:
Post a Comment