Wednesday, February 8, 2017

Jamhuri Kihwelu "Julio" Aomba Kibarua Simba

Kocha mkuu wa zamani wa klabu ya Mwadui ya mjini Shinyanga, Jamhuri Kihwelu, ameweka bayana kuwa yupo tayari kurudi kuitumikia Simba katika nafasi ya ukatibu mkuu.

Julio amesema kuwa hana wasiwasi na yupo tayari kuitumikia klabu hiyo endapo tu uongozi wa Simba utaridhia kumpa nafasi hiyo.

"Siyo kama najipigia chapuo lakini kama viongozi wa Simba wakiamua kunipa nafasi ya ukatibu sitaweza kukataa kwa sababu naipenda timu hiyo na kila mmoja anajua na kama nikiwepo naamini nitaongezea kitu fulani na kuifanya timu ipate matokeo mazuri"

Nafasi hiyo ilikuwa inashikiliwa na Patrick Kahemela ambaye kwa sasa amekuwa mkurugenzi wa michezo katika kituo cha runinga cha Azam. Aidha, Julio ameongeza kuwa, uzuri wake yeye ni kwamba hakufungiwa na mtu yeyote kujihusisha na mpira wa miguu isipokuwa ni yeye mwenyewe tu ndiye aliamua kukaa pembeni kutojihusisha na maswala hayo.

“Uzuri wangu kwangu kwamba sikufungiwa na mtu yeyote kujihusisha na soka hivyo hata nikirejea hakuna ambaye atashtuka na niwaahidi kwamba nitaitumikia nafasi hiyo kuleta mabadiliko yaliyoshindikana kwa kipindi kirefu,” alisema Julio akizungumza na Championi

Related Posts:

  • AZAM VS SIMBA KUPIGWA DIMBA LA UHURU Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kati ya Azam FC na Simba ya Dar es Salaam, utafanyika Jumamosi Septemba 17, 2016 kama ilivyopangwa awali. Ila mchezo huo utafanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam badala y… Read More
  • BOCCO AITISHIA NYAU SIMBA ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya kupambana na Simba, Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’, amesema kuwa wanamorali kubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo utakaofanyika … Read More
  • TAMBO ZINAZIDI NA MUDA UNAKARIBIA Read More
  • OMOG ASHUSHA PRESHA ZA WANAMSIMBAZI Kocha wa klabu ya Simba, Mcameroon, Joseph Omog amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kufuatia sare ya bila kufungana waliyoipata dhidi ya JKT Ruvu. Omog amesema hayo ni matokeo ya kawaida ya kimchezo hivyo mash… Read More
  • YANGA WAPATA ENEO LA UWANJA Hatimae yanga yapata kibali cha kujenga uwanja wao katika manispaa ya kigamboni baada ya kusubiri michakato kwa muda mrefu sana. hayo yamethibitishwa na mtu wa ndani wa kilabu ya yanga hapo jana. eneo hilo lina hekari zaid… Read More

0 comments:

Post a Comment