Saturday, February 4, 2017

chelsea vs Arsenal, Stamford Bridge




Ikiwa imetoka  kusuluhu na Liverpool, Chelsea itataka kujihakikishia nafasi ya kutwaa kombe pale tu itakapoweza kupata Matokeo chanya mbele ya Arsenal

Arsenal inaingia uwanjani Stamford Bridge kwa lengo moja la kuhakikisha inapunguza gepu la pointi na kufikia 6.

Mechi ya mwisho ya Epl Arsenal walikubali kipigo cha 2 -1 kutoka kwa Watford, wakati Chelsea wao walitoka sare ya 1 -1 na Liverpool .

Mchezo wa mwanzo uliozikutanisha Arsenal na Chelsea, Arsenal walitungua Chelsea 3 -0 katika dimba la Emirates magoli ya Alexis Sanchez, Theo Walcott na Mesut Ozil, hvyo leo Chelsea watahitaji kulipa kisasa ndani ya uwanja wao huku Arsenal wakitaka kulinda Heshima yao mbele ya Chelsea.



Mchezo huo utaanza saa 15:30 kwa saa za Afrika Mashariki.  

0 comments:

Post a Comment