Saturday, February 4, 2017

Samatta kazini leo Ubeligiji


KRC Genk leo inashuka katika dimba lake la nyumbani la Luminus Arena kumenyana na timu inayoburuza mkia katika Belgium - Pro League timu iitwayo Royal Excel Mouscron. Mchezo utakaopigwa saa 22:00 majira ya Afrka Mashariki.
Genk ipo nafasi ya 8 baada ya michezo 23 ikiwa na alam 34.

Mchezaji  Mbwana Samatta ambae anaiwakilisha vyema Tanzania kimataifa kwa sasa, yupo nafasi ya 15 pamoja na kiungo mshambuliaji wa Manchester City Kevin De Bruyne kwa upachikaji mabao katika historia ya KRC Genk kwa kutia kambani jumla ya magoli 17 huku anaeongoza akiwa na magoli 105 ambae anaitwa Jelle Vossen.

Hii ina maana kuwa endapo Samatta atafunga goli tatu leo atakuwa sawasawa na Christian Benteke ambae anakipiga katika klab ya Crystal Palace.


Kilalakheri Samatta katika mafanikio yako Watanzania tupo nyuma yako. 

0 comments:

Post a Comment