Monday, August 15, 2016

VIDEO:HALI ILIVYO MAKAO MAKUU YA YANGA BAADA YA MANJI KUTANGAZA KUJIUZULU

Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusuf Manji pamoja na makamu wake Clement Sanga wametangaza kujiuzulu nyadhifa zao kwa kile walichodai kuwa kusakamwa na matajiri wapenzi wa Yanga baada ya Manji kutangaza kutaka kuikodi Yanga kwa muda wa Miaka 10;

"Natukanwa sana na baadhi ya matajiri ambao ni wapenzi wa Yanga. . Hawapendi mimi niwepo pale. . Pesa ni yangu natoa kwa mapenzi niliyonayo kwa klabu yangu. . Kwanini nitukanwe wakati sipati maslahi yoyote?najiuzulu". . Ni kauli ya mwenyekiti wa Yanga SC ambaye ametangaza kujiuzulu kufuatia kusakamwa na hasa baada ya kuomba kuichukua Yanga kwa miaka 10.

Hata hivyo kumekuwa na vikao mbalimbali kumsihi Manji abadili maamuzi yake lakini inaonekana amechoka na ameamua kuibwaga Yanga.Tayari Reginald Mengi ameonesha nia ya kuingia Yanga endapo Manji ataondoka. . Leo jioni baraza la wazee wanataraji kuwa na kikao na Mengi.

 Taarifa za hivi punde ni kwamba ni kweli kwamba Mwenyekiti huyyo amekusudia kufanya hivyo kwa sababu anasakamwa , anatukanwa na kudhalilishwa na Makonda na Mzee Akilimali.

Lakini kibaya hakuna tamko kutoka kwa Mwana-Yanga yeyote aliyekemea hilo na kuonyesha kumuunga mkono Manji .Hivyo anajiona mnyonge na amesuswa bora akae pembeni. Viongozi wa Kanda wote wameamua kuitisha kikao cha Dharula kesho SAA 4 Asubuhi pale makao makuu ambapo litatoka tamko rasmi kuhusiana na taarifa hizo.

Tazama Video Hapa Chini Ujionee Hali Ilivyo Makao Makuu Ya Yanga Hivi Sasa;
 
Source:Naipenda Yanga Facebook Page
 Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook, Bonyeza  HAPA 

 

0 comments:

Post a Comment