Friday, July 1, 2016

MAN U WAANZA KUUZA JEZI NA. 9 YA IBRAHIMOVIC

Kwa mujibu wa ripoti zilizoenea sana siku za hivi karibuni ni kwamba Zlatan Ibrahimovic anakaribia kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Man U.

Tangu aondoke PSG kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu wa 2015/16, Zlatan amekuwa akihusishwa sana na kujiunga na United.

Zlatan na Mourinho wamewahi kufanya kazi pamoja katika klabu ya Inter Milan na tangu wakati huo Zlatan amekuwa akimsifia sana Mourinho.

Kwa mujibu wa ripoti ya BBC ni kwamba Zlatan anatarajiwa kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa Man U mwishoni mwa wiki hii.

Siku ya Alhamisi ziliibuka picha za jezi namba tisa zilizoandikwa jina la Ibrahimovic zikiuzwa katika duka la klabu hiyo.

Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook


0 comments:

Post a Comment