Wednesday, July 6, 2016

KOCHA WA ARGENTINA ABWAGA MANYANGA

Gerardo Martino ameamua kuachana na kibarua cha kuifundisha timu ya taifa ya Argentina kufuatia matokeo mabaya Copa America 2016.

Moja ya sababu zilizomfanya Martino kuachia nafasi hiyo ni ugumu wa kuwapata wachezaji wazuri ambao wangewakilisha Argentina katika kwenye Olimpiki 2016 wiki chache kabla ya mashindano hayo kuanza.

Argentina imepoteza fainali 3 hadi, fainali mbili za Copa America dhidi ya Chile na fainali moja ya kombe la dunia 2014 dhdi ya Ujerumani.

Martino ambaye amewahi kuifundisha Barcelona msimu wa 2013/14 kwa sasa atakuwa tayari kutafuta changamoto mpya, huku pia Javier Mascherano nae akiamua kukaa pembeni kuitumikia timu yake ya taifa.

Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook


0 comments:

Post a Comment