Monday, July 11, 2016

JERRY MURO ATAKIWA KUWA NA ADABU

Sakata la Ofisa habari wa Yanga Jerry Muro kufungiwa mwaka mmoja kutojihusisha na maswala ya soka pamoja na kupigwa faini ya sh. Milioni tatu limechukua sura mpya baada ya viongozi wa TFF kujibu kauli za Msemaji huyo.
Katibu Mkuu Wa TFF, Selestine Mwesigwa

Suala hilo limechukua sura mpya baada ya TFF kumtaka Jerry Muro kuwa na adabu huku wakisema kuwa adabu hainunuliwi dukani. Hayo yamesemwa na katibu mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa kufuatia kauli za Jerry Muro kuwa TFF imekurupuka na kwamba haizingatia haki za kibinadamu wakati wakitoa adhabu hiyo.

kwa upande mwingine Ofisa habari wa shirikisho hilo, Alfred Lucas ameonyesha kushangazwa na kauli kali anazozitoa Jerry Muro huku akisema kuwa TFF imeshafunga mjadala wa suala hilo.

"Hukumu ishatoka, alishapewa nakala ya hukumu yake, yeye kama anaendelea kutoa lugha za kukashifu, muache aendelee sisi kwa upande wa TFF tulishalifunga suala hilo" alisema Lucas.

Viongozi wa TFF wameamua kutoa kauli hizo kwa kile kilichodaiwa na Jerry Muro kuwa yeye ana akili nyingi zaidi kuliko viongozi wa TFF na kutaka wasimsumbue kwa kuwa yeye si mwanachama wa TFF.
Ofisa habari huyo wa Yanga alienda mbali zaidi na kuanza kuhoji elimu ya viongozi hao wa TFF.

Hata hivyo, pamoja na Muro kudai kuwa yeye ni muajiriwa na si mwanachama wa TFF, Yanga ni mwanachama wa Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), CAF, FIFA na TFF, yeyote kiongozi wa Yanga anaweza kuadhibiwa na mashirikisho hayo kwa kuwa msemaji wa klabu ni agizo la Fifa ambalo lipo ndani ya katiba za wanachama wake na wanachama wa shirikisho husika.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook

Related Posts:

  • Joseph Kimwaga Ajutia Kutua Msimbazi kimwaga Kushoto akishangilia goli Sraika wa Simba, Joseph Kimwaga ametamka kuwa kati ya vitu ambavyo anajutia kwenye maisha yake ya soka, basi ni kutua kuichezea timu hiyo.Mshambuliaji huyo alitua kuichezea Simba kwen… Read More
  • Hizi Ndio Mbinu Zitakazowaua Al Ahly Taifa Kocha Mkuu wa Yanga YANGA inajiandaa kufungasha virago vyao kutoka Kisiwani Pemba ilipoenda kujichimbia kwa siku chache kujiandaa na mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini ikiwa huko Vijana wa Jangwani wamepewa mbin… Read More
  • Kikosi Cha Esperance De Tunis Kutua Nchini Leo Kikosi Cha Esperance De Tunis Azam inatarajia kuvaana na Esperance katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika, mechi ambayo itachezwa kwenye Uwanja wa Chamazi, keshokutwa Jumapili. Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saadi Kawemb… Read More
  • Yaliyosemwa Na TFF Kuhusu Yanga Na Azam Haya Hapa Rais Wa TFF Jamali Malinzi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezitakia kila la kheri klabu za Azam FC na Young Africans ambao ni wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa itayochezwa wikiendi hii. TFF i… Read More
  • Wadhamini Wa UEFA Kuboresha Soka La Tanzania Shirikishio la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeishukuru kampuni ya bia ya Heineken ambao ni wadhamini wakuu wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya (UEFA) kwa kujitolea kufanya ukarabati wa viwanja vitatu vya mpira w… Read More

0 comments:

Post a Comment