Friday, July 1, 2016

JAMES RODRIGUEZ AITAJA KLABU ANAYOTAKA KUHAMIA

James Rodriguez amesema anataka kujiunga na wababe wa soka la Ufaransa klabu ya Paris Saint-Germain msimu ujao.

Rodriguez alikuwa akihusishwa sana kutimkia ligi kuu ya Uingereza lakini amesema anatamani kujiunga na PSG.

Mkolombia huyo amekuwa akitumikia muda wake mwingi benchi katika klabu yake ya Madrid chini ya kocha Zidane hivyo kutaka kutimka klabuni hapo na kwenda kujaribu kwingine.
Kwa mujibu wa Mirror, Rodriguez amewashiwa taa za njano klabuni hapo na anaweza kujiunga na klabuu yoyote apendayo.

Kuwasili kwa Jose Mourinho Manchester United kulipelekea baadhi ya watu kumuhusisha Rodriguez kujiunga na mashetani wekundu huku pia klabu za Manchester City na Chelsea zikionyesha kuhitaji huduma ya Winga huyo.

Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook

Related Posts:

  • CHIRWA ATUA JANGWANI KWA SH. MILIONI 240Mshambuliaji raia wa Zambia, Obrey Chirwa amejiunga na Yanga kwa dau la sh. Milioni 240 akitokea katika klabu ya FC Platinum za Zimbabwe. Chirwa ameifungia Platinum mabao matano katika mechi nane alizocheza kwenye ligi kuu… Read More
  • KIUNGO MPYA SIMBA TISHIO KWA MKUDE, NDEMLASimba imefanikiwa kumsajili Kiungo Mzamiru Yasini akitokea katika klabu ya Mtibwa Sugar. Yasini amesema hayupo tayari kukaa benchi hivyo atahakikisha anapambana na wakongwe ili kujihakikishia nafasi yake katika kikosi cha … Read More
  • KOCHA MWENYE REKODI ZA KIMATAIFA KUTUA SIMBAHarakati za usajili katika klabu ya Simba bado zinaendelea na habari za hivi karibuni zinasema makocha wanne kutoka katika nchi nne tofauti wamejitokeza kutaka kuinoa klabu hiyo. Geofrey Nyange "Kaburu" (Makamu mwenyekiti … Read More
  • "SINA MPANGO WA KUHAMIA SIMBA" JEBAKiungo Ibrahimu Jeba wa klabu ya Mtibwa Sugara amesema hana mpango wa kuihama Mtibwa Sugar kwa sasa. Simba walionyesha nia ya kumuhitaji kiungo huyo lakini yeye mwenyewe amedai hana mpango wa kuhamia klabu hiyo, Jeba amese… Read More
  • UKIMYA WA VIONGOZI WAMFANYA BEKI ASAKE KLABU SIMBAMiraji Adam ni mchezaji wa Simba ambaye alikuwa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Coastal Union ambayo kwa sasa imeshuka daraja huku yeye akisema yupo tayari kucheza katika klabu yoyote. Mkataba wa Miraji na Simba unaelek… Read More

0 comments:

Post a Comment