Wednesday, July 13, 2016

AZAM MEDIA YAZIMWAGIA VILABU VYA VPL MAMILION

Kampuni ya Azam Media imeongeza mkataba wa kurusha mechi za ligi kuu Vodacom msimu ujao 2016/17.

Mkataba huo umesainiwa jana kati ya TFF na klabu ya bodi ya Ligi na Uongozi wa Azam, huku mkataba huo ukiwa umeboreshwa kidogo kwa klabu kupata kiasi cha Sh. Milioni 126 kwa mwaka.

Awali kila klabu ilikuwa inapata sh. milioni 100. Hata hivyo klabu ya Yanga imezisusia klabu hizo kwa kile wanachodai kuwa hawawezi kupata sawa na klabu nyingine kutokana na ukubwa wa klabu yao na kwamba wana uwezo wa kuingiza zaidi ya fedha hizo kwenye mchezo wao mmoja dhidi ya Simba.

Katika mkataba huo kila klabu itapata sh. milioni 42 kwa awamu tatu ambapo jumla yake inakuwa milioni 126, Lakini awamu ya tatu ambayo ndio ya mwisho itatolewa kwa mfumo tofauti ambao utakuwa timu inayoshika nafasi ya juu katika msimamo wa ligi itafaidika kwa kupata zaidi na itakuwa hivyo hadi kwa klabu inayoshika nafasi ya chini.

Akizungumza jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tan zania (TFF), Selestine Mwesigwa alisema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha kunakuwa na ushindani katika ligi.

“Kila timu inatakiwa kujiandaa vya kutosha na kuleta ushindani, kuona umuhimu wa kukaa kileleni, kila timu iwe na hamu ya kushinda mechi zake ili mwisho wa siku ifaidike,” alisema.

Kwa upande wake, mkurugenzi wa Azam Tiddo Muhando alisema kampuni yake imeamua kuongeza zawadi na kubadilisha mfumo wa utoaji ili kuongeza ushindi na kampuni yake itaonesha ligi hiyo kwa kiwango cha juu tofauti na msimu uliopita.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook

Related Posts:

  • Hapatoshi Leo Tena Taifa Patashika za ligi kuu ya kandanda tanzania bara zinaendelea tena leo kwa mchezo mmoja tu kupigwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha wenyeji Simba SC dhidi ya Toto Africans ‘wana kishamapanda’kutok… Read More
  • Tambwe Amechuja Awekwe Benchi Mashabiki wa Klabu ya Dar Young Africans wameonyesha kutokufurahishwa na kiwango kinachoonyeshwa na mshambuliaji wao Amis Tambwe siku za hivi karibuni. Tambwe ambe ana magoli 18 katika orodha ya wafungaji bora msimu huu an… Read More
  • Hiki Ndio Kikosi Cha Yanga Leo Dhidi Ya Mtibwa Sugar LIGI KUU || TZ - BARA || 2015~2016. YANGA SC Vs MTIBWA SUGAR FC. UWANJA - Uwanja wa Taifa. Muda - saa 10 : 00Alasiri. >>>>>>KIKOSI CHA YANGA LEO<<<<<<<< 1. Deogratias Bonave… Read More
  • Mnyama Achinjwa Taifa Timu ya soka ya Simba imezidi kupoteza matumaini ya kunyakua ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kukubali kichapo cha Goli 1 - 0 toka kwa Toto Africans ya Mwanza.Katika mchezo huo ambao wadau wengi wa soka waliip… Read More
  • Abdi Banda Alia Na Viongozi Wa Simba Mchezaji wa Simba Abdi Banda anasema hajui mustakabali wake katika Klabu hiyo kufuatia tamko la adhabu aliyopewa kutokana  na kupishana kauli na kocha wake Jackson Mayanja katika mechi dhidi ya Coastal Union. Ana… Read More

0 comments:

Post a Comment