Friday, May 20, 2016

FIFA YAPELEKA SEMINA YA CLUB LICENSING ETHIOPIA

Wawakilishi wa Vilabu na Vyama Vya Mpira kutoka pande zote za Afrika watakutana Jijini Addis Ababa, Ethiopia wiki hii kwa ajili ya semina ya Club Licensing.



Wawakilishi wa Vilabu na Vyama Vya Mpira kutoka pande zote za Afrika watakutana Jijini Addis Ababa, Ethiopia wiki hii kwa ajili ya semina ya Club Licensing inayoendeshwa na Shirikisho la mpira wa miguu Duniani FIFA ikishirikiana na Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF.

Lengo la semina hiyo ni kutekeleza mfumo wa Club Licensing duniani kote pamoja na kuzifanya klabu zijiendeshe kisasa zaidi katika nyanja zote zikiwemo kiufundi, kifedha na kiutawala. Semina hiyo itahusisha wawakilishi waandamizi kutoka nchini za Misri, Ethiopia, Gambia, Ghana, Kenya, Liberia, Libya, Nigeria, Somalia, South Afrika, Sudan na Tanzania katika kujulishana uzoefu  na kupeana njia bora za jinsi ya kuziendesha klabu kitaalam katika Afrika.

"Huu ni mpango mzuri unaowapa wanachama wote shiriki pamoja na vilabu, Ligi na wachezaji watakaohudhuria, zana za msingi zinazohitajika kutekeleza Club Licensing" alisema Salihu Abubakar Mtendaji Mkuu wa chama cha wachezaji wa kulipwa cha nchini Nigeria.

Nae Mkuu wa idara ya wachezaji wa kulipwa FIFA, James Johnson alisema, huu mfumo wa Club Licensing ulishaanza kufanya kazi na CAF huku vilabu 61 kutoka katika nchi 26 wakiwa wanachama.

Semina hiyo inakuwa ni mara ya pili kwa FIFA kufanya barani Afrika mwaka 2016.Uzinduzi wa Seminar hizi ulifanyika nchini Afrika Kusini na baadae seminar hizi zitafanyika nchini Morocco na Cameroon. Semina hizi pia zinafanyika katika maeneo mbalimbali duniani katika kipindi chote cha mwaka.

Related Posts:

  • LEWANDOWSKI AIFIKIA REKODI ILIYOWEKWA MIAKA 39 ILIYOPITA MCHEZAJI wa zamani wa klabu ya Borrusia Dortmund anayekipiga katika klabu ya Bayern Munich kwa sasa Robert Lewandowski amefikia rekodi iliyowekwa miaka 39 iliyopita katika ligi kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundeslig… Read More
  • HATIMA YA VAN GAAL MAN UNITED YAWEKWA WAZI Louis Van Gaal amehakikishiwa na mabosi wa United kuwa ataendelea kubaki katika klabu hiyo hadi mwisho wa mkataba wake kwa mujibu wa ripoti ya Daily Star. Mdachi huyo anayeinoa United amekuwa akisemwa sana juu ya uwezo … Read More
  • ARSENE WENGER KUSAINI MKATABA MWINGINE NA ARSENAL Uongozi wa klabu ya Arsenal umepanga kumwongeza mkataba wa miaka 2 kocha wake Arsene Wenger mkataba ambao anatarajiwa kusaini October mwaka huu, lengo likiwa ni kupata muda wa kutosha wa kumtafuta atakaekuwa mrithi wa We… Read More
  • SUPER MARIO AKUBALI KUJIUNGA NA MAN UNITED Manchester United wanakaribia kumalizana na mchezaji wa Sporting Lisbon Joan Mario. Mabosi wa United wamefanya mazungumzo mara kadhaa na mchezaji huyo mwenye miaka 23 raia wa Ureno na wakala wake anaamini dili hilo li… Read More
  • KLABU 5 TAJIRI ZAIDI DUNIANI 2016 Real Madrid imetajwa kuwa ndio klabu tajiri zaidi duniani kwa mara ya 4 mfululizo, kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Forbes. Wababe hao wa Hispania Walibeba taji la Uefa Super Cup na Klabu Bingwa duniani (Fifa Club W… Read More

0 comments:

Post a Comment