Sunday, April 24, 2016
Home »
Kimataifa
,
Laliga
» Zinedine Zidane Akwepa Uvumi Unaomhusisha James Rodriguez Kuondoka Madrid
Zinedine Zidane Akwepa Uvumi Unaomhusisha James Rodriguez Kuondoka Madrid
kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekwepa kutolea maelezo uvumi unaosambaa kuhusu mchezaji wake James Rodriguez kuihama klabu hiyo.
James amekuwa akisugua benchi siku za hivi karibuni hali ambayo inazua mijadala kwa wapenzi wa mchezaji huyo. katika mchezo wa jana dhidi ya Rayo Vallecano James alitokea benchi Madrid ikishinda kwa magoli 3 - 2.
"sioni tatizo lolote kwa James, ni mchezaji mzuri na ni mchezaji muhimu pia kwa klabu, alicheza vizuri na alifunga goli katika mchezo wetu dhidi ya Eibar na Getafe. Na anahitaji kucheza mechi nyingi zaidi, lakini hali hiyo inamkuta kila mchezaji ambae huwa hajacheza kwa muda mrefu. Nina wachezaji 24 katika kikosi changu na nahitaji kuwachagua 11 tu kati ya hao, muda mwingine inaonekana kama nahitaji kufanya mabadiliko matatu katika kila mchezo, lakini nitafanya hivyo endapo tu nitaona ulazima wa kufanya hivyo, mimi ndio kocha na ndio nafanya maamuzi" alisema Zidane
Inasemekana James alikuwa na mahusiano mazuri sana na Kocha Rafael lakini tangu kuja kwa Zidane muda mwingi amekuwa akikaa benchi na katika mechi 8 za hivi karibuni za Real Madrid, James ameanza kikosi cha kwanza katika mechi mbili tu.Hali hii ndo inayoleta uvumi wa kwamba huenda Mkolombia huyo akaondoka klabuni hapo.
pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com
Related Posts:
Zinedine Zidane Akwepa Uvumi Unaomhusisha James Rodriguez Kuondoka Madrid kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekwepa kutolea maelezo uvumi unaosambaa kuhusu mchezaji wake James Rodriguez kuihama klabu hiyo. James amekuwa akisugua benchi siku za hivi karibuni hali ambayo inazua mijadala kwa w… Read More
MBIO ZA UBINGWA LA LIGA ZAZIDI KUWA NGUMU Barcelona inazidi kubaki kileleni kwa tofauti tu ya magoli na Atletico huku zikiwa zimebaki mechi mbili tu kumaliza msimu baada ya ushindi wao wa jana wa 2 – 0 magoli yaliyofungwa na Rakitic na Luis Suarez dhidi ya Real … Read More
Gareth Bale Asisitiza Hana Bifu Na Christiano Ronaldo Gareth Bale amekanusha uvumi unaomhusisha yeye kutokuwa na mahusiano mazuri na mchezaji mwenzie Christiano Ronaldo maarufu kama CR7, akisema ana mahusiano mazuri tu na mchezaji huyo na kamwe hajawahi kuingia katika mzozo… Read More
Mkataba Wa Neymar Barcelona Wavuja Mbrazil Neymar ni Mchezaji wa karibuni zaidi Mkataba wake kuvuja akiwa Barcelona baada ya Mtandao wa Football Leaks kuweka wazi mkataba wake mpya Camp Nou. Mchezaji huyo alihamia Barcelona akitokea Santos ya Nchini Brazil a… Read More
Mengine Yakustaajabisha Yanayomhusu Neymar Jr Ni mara chache sana hutokea mtu kumsikitikia mchezaji Mkubwa anaepata kipato kidogo, lakini habari zilizovuja hivi punde kupitia mtandao wa Football Leaks zinaonyesha kwamba Neymar anapata Sh. Milioni 240 kw… Read More
0 comments:
Post a Comment