Sunday, April 24, 2016

Zinedine Zidane Akwepa Uvumi Unaomhusisha James Rodriguez Kuondoka Madrid


kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekwepa kutolea maelezo uvumi unaosambaa kuhusu mchezaji wake James Rodriguez kuihama klabu hiyo.

James amekuwa akisugua benchi siku za hivi karibuni hali ambayo inazua mijadala kwa wapenzi wa mchezaji huyo. katika mchezo wa jana dhidi ya Rayo Vallecano James alitokea benchi Madrid ikishinda kwa magoli 3 - 2.

"sioni tatizo lolote kwa James, ni mchezaji mzuri na ni mchezaji muhimu pia kwa klabu, alicheza vizuri na alifunga goli katika mchezo wetu dhidi ya Eibar na Getafe. Na anahitaji kucheza mechi nyingi zaidi, lakini hali hiyo inamkuta kila mchezaji ambae huwa hajacheza kwa muda mrefu. Nina wachezaji 24 katika kikosi changu na nahitaji kuwachagua 11 tu kati ya hao, muda mwingine inaonekana kama nahitaji kufanya mabadiliko matatu katika kila mchezo, lakini nitafanya hivyo endapo tu nitaona ulazima wa kufanya hivyo, mimi ndio kocha na ndio nafanya maamuzi" alisema Zidane

Inasemekana James alikuwa na mahusiano mazuri sana na Kocha Rafael lakini tangu kuja kwa Zidane muda mwingi amekuwa akikaa benchi na katika mechi 8 za hivi karibuni za Real Madrid, James ameanza kikosi cha kwanza katika mechi mbili tu.Hali hii ndo inayoleta uvumi wa kwamba huenda Mkolombia huyo akaondoka klabuni hapo.







pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment