Thursday, April 28, 2016

Mamadou Sakho Afungiwa Kucheza Mpira


Beki wa Liverpool amekataa kuchukuliwa vipimo kwa mara ya pili baada ya majibu ya vipimo vya kwanza kuonyesha alikuwa anatumia dawa za kupunguza unene ambazo haziruhusiwi kwa wanamichezo. Kukataa huko kumelifanya shirikisho la Mpira barani ulaya UEFA kumfungia mchezaji huyo kwa muda wa siku 30.
UEFA wamesema katika tovuti yao kuwa “hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho kufuatia vipimo vilivyofanyika katika mechi ya UEFA Europa League raundi ya 16, katika mchezo wa pili kati ya Mancester United na Liverpool  iliyochezwa March 17 mwaka huu”.

UEFA wamesisitiza kuwa hatua zaidi za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya mchezaji huyo hasa baada ya kukataa kufanyiwa vipimo kwa mara ya pili.


Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • NYOTA WA ZAMANI WA MAN UNITED AITABIRA UBINGWA CHELSEA Paul Scholes anasema Chelsea wana nafasi ya kuibuka mabingwa wa ligi kuu Nchini Uingereza. Chelsea inaongoza ligi hiyo kufuatia ushindi mnono katika mechi zake tatu ambazo imekwishacheza hadi hivi sasa chini ya kocha Mpya… Read More
  • AUBAMEYANG AITAMANI REAL MADRID Hakuna ubishi kuwa Nyota wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang anatamani kujiunga na miamba ya soka ya nchini Hispania klabu ya Real Madrid. Aubameyang amewahi kumuahidi babu yake kuwa ipo siku atakuja kucheza k… Read More
  • WAAMUZI MECHI KATI YA TANZANIA DHIDI YA IVORY COAST Mchezo Mpira wa Miguu wa Ufukweni kati ya Tanzania na Ivory Coast kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa utachezeshwa na waamuzi kutoka Uganda ambao ni Shafic Mugerwa katikati na wasaidizi wake ni Ivan Bayige … Read More
  • MAISHA YA FABREGAS CHELSEA YAFIKA UKINGONI Cesc Fabregas ameambiwa na kocha wa klabu ya Chelsea Antonio Conte kuwa anaweza kuondoka klabuni hapo. Conte ametoa kauli hiyo huku kukiwa kumebaki siku 2 tu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya. Kiungo h… Read More
  • Rasmi: Wilfred Bony Atua Stoke City Klabu ya Stoke City imekamilisha uhamisho wa Wilfred Bony kwa mkopo akitokea klabu ya Manchester City. Bony aliyefeli kumshawishi kocha mpya wa City, Mhispania Pep Guardiola amefanikiwa kufunga magoli 11 katika michezo 4… Read More

0 comments:

Post a Comment