Thursday, April 28, 2016

Mamadou Sakho Afungiwa Kucheza Mpira


Beki wa Liverpool amekataa kuchukuliwa vipimo kwa mara ya pili baada ya majibu ya vipimo vya kwanza kuonyesha alikuwa anatumia dawa za kupunguza unene ambazo haziruhusiwi kwa wanamichezo. Kukataa huko kumelifanya shirikisho la Mpira barani ulaya UEFA kumfungia mchezaji huyo kwa muda wa siku 30.
UEFA wamesema katika tovuti yao kuwa “hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho kufuatia vipimo vilivyofanyika katika mechi ya UEFA Europa League raundi ya 16, katika mchezo wa pili kati ya Mancester United na Liverpool  iliyochezwa March 17 mwaka huu”.

UEFA wamesisitiza kuwa hatua zaidi za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya mchezaji huyo hasa baada ya kukataa kufanyiwa vipimo kwa mara ya pili.


Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment