Monday, April 25, 2016

Gareth Bale Asisitiza Hana Bifu Na Christiano Ronaldo


Gareth Bale amekanusha uvumi unaomhusisha yeye kutokuwa na mahusiano mazuri na mchezaji mwenzie Christiano Ronaldo maarufu kama CR7, akisema ana mahusiano mazuri tu na mchezaji huyo na kamwe hajawahi kuingia katika mzozo na Ronaldo.

Wawili hao wanaunda timu hatari sana ya ushambuliaji Santiago Bernabeu, Bale alivunja rekodi ya dunia ya usajili iliyowekwa na Ronaldo wakati akihama kutoka Tottenhama kwenda Madrid mwaka 2013, lakini Muwelshi huyo (Bale) amesisitiza hana tatizo na Ronaldo.

Bale na Ronalo wanatarajiwa kufanya makubwa katika mchezo wao na Manchester City katika hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya UEAFA Champions League jumanne hii.

Akihojiwa kwenye interview Bale alisema “Yeye (Ronaldo) anazungumza kiingereza, kitu ambacho kilinisaidi sana nilipofika hapa (Madrid). Sisi pia (Bale na Ronaldo) wote tumetokea katika ligi moja ya Uingereza” .
“hatujawahi kuwa na tatizo, sijawahi kuzozana na Ronaldo, ni mtu mzuri sana na anapokuwa uwanjani anafanya vizuri sana na kila mmoja analijua hilo”
“watu muda mwingine wanapenda kupotosha mambo, hatujawahi kuingia katika mgogoro” alisema Bale.

Bale na Ronaldo wote wanafahamika kwa ufundi wao wa kupiga mipira ya adhabu (free kick) na Bale alisema alipata Ujuzi huo kupitia mafunzo ya pamoja na Ronaldo.


“Inafahamika wazi kuwa mipira ya adhabu ya upande wa kushoto ni ya Ronaldo na mipira ya adhabu ya upande wa kulia ni ya kwangu katika kila mchezo. Hivyo tunajua kisawasawa nini tunakifanya” aliongeza Bale ambae juzi ameisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa goli 3 -2 dhidi ya Rayo Vallecano, mechi ambayo Ronaldo hakucheza kutokana na maumivu ya msuli.


Bale, Benzema na Christiano Ronaldo wamepewa jina la BBC kutokana na uwezo wao wa ufungaji katika klabu ya Madrid



Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com 

Related Posts:

  • HUYU NDO KOCHA MPYA BRAZILTite ametajwa kuwa kocha mpya wa Brazil baada ya Dunga kutupiwa virago kufuatia matokeo mabovu waliyoyapata Brazil Copa America 2016. Tite Tite 55, anachukua nfasi ya Dunga aliyetimuliwa mara baada ya Brazil kutolewa hatu… Read More
  • ARGENTINA YATINGA FAINALI MESSI AWEKA REKODI COPA AMERICA Lionel Messi ameweka Rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika kikosi cha Argentina baada ya kufunga goli katika mechi ya robo fainali michuanoo ya Copa America dhidi ya Marekani, Mechi iliyomalizika alfajiri ya Le… Read More
  • IBRAHIMOVIC ATANGAZA KUSTAAFU SOKAZlatan Ibrahimovic 34, amesema atastaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya kumalizika kwa michuano ya Euro 2016' Ibrahimovic amesema mechi yake ya mwisho ni kati ya Sweden na Ubelgiji itakayochezwa Jumatano. Sweden it… Read More
  • YANGA TAYARI KWA KUIVAA MO BEJAIA Timu Ya Yanga imeshawasili nchini Algeria tayari kwa kuwavaa MO Bejaia katika mchezo wa kwanza hatua ya makundi kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, utakaofanyika siku ya kesho Jumapili juni 19, 2016 … Read More
  • MEDEAMA SC KUJITOA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA (CAF CC)Medeama huenda ikajitoa katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika CAF CC, kutokana na hali ngumu ya kifedha. Medeama imepangwa kucheza na TP-Mazembe katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo Juni 19,2016. CAF bado h… Read More

0 comments:

Post a Comment