Tuesday, January 31, 2017

Mkwasa Arejea Yanga

Charles Boniface Mkwasa ameteuliwa kuwa katibu mkuu Yanga Afrika kwa mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa katibu mkuu Baraka Deusdedit anarejea katika nafasi yake ya awali ya utunza fedha.

Akizungumza baada ya kurejea kikosini hapo Mkwasa amesema hana nia ya kukalia kiti cha ukocha tena kwani ana imani kubwa na walimu waliopo hivi sasa.

"Nimekuja Yanga Sc kufanya muunganiko kati ya waalimu na Sekretarieti na pia sina nia yeyote ya kurudi kwenye kiti cha kufundisha kwenye klabu ya Yanga SC kwani sina shaka yeyote juu ya walimu waliopo kwenye benchi la ufundi"

0 comments:

Post a Comment