Monday, July 11, 2016

ALICHOPOST MOURINHO INSTAGRAM BAADA YA URENO KUTWAA EURO

Katika kuonyesha furaha yake Jose Mourinho kufuatia ushindi walioupata Ureno katika fainali ya Euro 2016, Kocha huyo wa Man United amepost picha huku akiisindikiza na maneno yanasomeka hivi;  "Kama unataka kutembelea taifa la mabingwa wa Ulaya, tembelea Ureno"

Mourinho aliwahi kuingoza FC Porto mwaka 2004 kushinda taji la klabu bingwa barani ulaya (UEFA Champions League)  wakati ambao Porto ilikuwa ikichukuliwa kama kibonde kwenye mashindano hayo.

Ureno imeshinda mechi moja tu ndani ya dakika 90 za mchezo katika mechi zote walizocheza katika michuano ya Euro 2016, huku ikitoa sare tatu katika hatua ya makundi na ushindi ndani ya dakika 30 za nyongeza dhidi ya Crotia na Ufaransa pamoja na Penati dhidi ya Poland.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook

0 comments:

Post a Comment