Marouane Fallaini ameweka wazi kuwa Kocha Jose Mourinho alimtumia ujumbe alipowasili Man United.
Kiungo huyo wa Ubelgiji amesema Mourinho alimtumia ujumbe akimkaribisha United huku pia akimtakia kila la kheri katika michuano ya Euro
"Mourinho aliwasiliana na mimi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS), akinikaribisha United na kunitakia Euro njema" alisema Fellaini alipokuwa katika mazoezi ya timu yake ya taifa jana jumamosi.
Fellaini alisema amefurahishwa na ujio wa kocha Mourinho klabuni United na kwamba yupo tayari kufanya kazi chini ya kocha huyo.
"Anapenda kushinda mataji na itakuwa ni heshima kubwa kwangu kufanya kazi na yeye. Sasa kazi ipo kwangu kumfanya aniamini na kunipanga kikosi cha kwanza" aliongeeza Fellaini.
Ujio wa Mourinho Man Utd umepokelewa kwa hisia tofauti na wachezaji wa klabu hiyo, kwani wapo ambao kuchukua kwake mikoba klabuni hapo ndio kunahitimisha uwepo wao United huku wengine wakifurahia baada ya kuhakikishiwa kuendelea kuwepo klabuni hapo.
Wachezaji ambao tayari Mourinho ameshaonyesha kutokuwahitaji klabuni Hapo ni Daley Blind, pamoja na Nick Powell na huenda idadi hiyo ikaongezeka.
==============
Bonyeza hapa ku-Like Page yetu ya Facebook
==============
Sunday, June 12, 2016
MAROUANE FELLAINI:"HIKI NDO ALICHONIAMBIA MOURINHO"
Related Posts:
HUU NDO USAJILI WA KWANZA WA MOURINHO MAN U Mlinzi wa kati wa klabu ya Villarreal ya nchini Hispania Eric Bailly huenda akawa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Mourinho katika klabu ya Man United. Ripoti kutoka ndani ya klabu ya Man U zinasema wameshafikia makubali… Read More
MASHABIKI WA LEICESTER CITY WAMJIA JUU MKEWE VARDY NAE AWAJIBU Habari kubwa za usajili kwa sasa barani ulaya ni pamoja na ile inayomuhusisha Jamie Vardy kujiunga Arsenal na taarifa hizo zimepokelewa vibaya na mashabiki wa Leicester City. Straika huyo wa Leicester anatarajiwa ku… Read More
HUYU NDO ANAETARAJIWA KUCHUKUA MIKOBA YA KOCHA JACKSON MAYANJA SIMBA Simba ipo katika harakati za kukisuka upya kikosi chao na tayari wapo katika mazungumzo na kocha Mzimbabwe Kalisto Pasuwa. Mwenyekiti wa kamati ya Usajili Simba Zacharia Hans Pope yupo katika mazungumzo ya mwisho na koch… Read More
BEKI KISIKI WA GORMAHIA AOMBA KUJIUNGA NA SIMBA SC AJE KUONYESHA KAZI Beki wa Gormahia ya nchini Kenya Karim Nzigiyimana ameweka wazi kuwa yupo tayari kujiunga na Simba SC, kwani kwa muda mrefu amekuwa akitamani kucheza Ligi kuu Nchini Tanzania. Karim Nzigiyimana amesema yupo tayari kujiun… Read More
ZLATAN IBRAHIMOVIC ATAJA TAREHE ATAKAYOTANGAZA TIMU ANAYOJIUNGA NAYO Straika Mswedish Zlatan Ibrahimovic aliyekataa kuongeza mkataba na klabu yake ya PSG amesema ifikapo Juni 7, 2016 ndipo ataweka wazi klabu ambayo anajiunga nayo. Zlatan Ibrahimovic anatarajia kutangaza wapi anatarajia kwe… Read More
0 comments:
Post a Comment