Sunday, June 12, 2016

MAROUANE FELLAINI:"HIKI NDO ALICHONIAMBIA MOURINHO"

Marouane Fallaini ameweka wazi kuwa Kocha Jose Mourinho alimtumia ujumbe alipowasili Man United.

Kiungo huyo wa Ubelgiji amesema Mourinho alimtumia ujumbe akimkaribisha United huku pia akimtakia kila la kheri katika michuano ya Euro

"Mourinho aliwasiliana na mimi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS), akinikaribisha United na kunitakia Euro njema" alisema Fellaini alipokuwa katika mazoezi ya timu yake ya taifa jana jumamosi.

Fellaini alisema amefurahishwa na ujio wa kocha Mourinho klabuni United na kwamba yupo tayari kufanya kazi chini ya kocha huyo.

"Anapenda kushinda mataji na itakuwa ni heshima kubwa kwangu kufanya kazi na yeye. Sasa kazi ipo kwangu kumfanya aniamini na kunipanga kikosi cha kwanza" aliongeeza Fellaini.

Ujio wa Mourinho Man Utd umepokelewa kwa hisia tofauti na wachezaji wa klabu hiyo, kwani wapo ambao kuchukua kwake mikoba klabuni hapo ndio kunahitimisha uwepo wao United huku wengine wakifurahia baada ya kuhakikishiwa kuendelea kuwepo klabuni hapo.

Wachezaji ambao tayari Mourinho ameshaonyesha kutokuwahitaji klabuni Hapo ni Daley Blind, pamoja na Nick Powell na huenda idadi hiyo ikaongezeka.
==============
 Bonyeza hapa ku-Like Page yetu ya Facebook
==============

Related Posts:

  • Rasmi: Wilfred Bony Atua Stoke City Klabu ya Stoke City imekamilisha uhamisho wa Wilfred Bony kwa mkopo akitokea klabu ya Manchester City. Bony aliyefeli kumshawishi kocha mpya wa City, Mhispania Pep Guardiola amefanikiwa kufunga magoli 11 katika michezo 4… Read More
  • MAISHA YA FABREGAS CHELSEA YAFIKA UKINGONI Cesc Fabregas ameambiwa na kocha wa klabu ya Chelsea Antonio Conte kuwa anaweza kuondoka klabuni hapo. Conte ametoa kauli hiyo huku kukiwa kumebaki siku 2 tu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya. Kiungo h… Read More
  • Arsenal Yakamilisha Usajili Wa Shkodran Mustafi Klabu ya Arsenal imetangaza rasmi kumsajili beki wa kati wa Valencia Shkodran Mustafi kwa ada ya uhamisho ambayo haijawekwa wazi. Licha ya thamani ya uhamisho wa mchezaji huyo kutowekwa wazi lakini habari za chini chini z… Read More
  • AUBAMEYANG AITAMANI REAL MADRID Hakuna ubishi kuwa Nyota wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang anatamani kujiunga na miamba ya soka ya nchini Hispania klabu ya Real Madrid. Aubameyang amewahi kumuahidi babu yake kuwa ipo siku atakuja kucheza k… Read More
  • WEST BROM YAVUNJA REKODI YA KLABU USAJILI WA CHADLI Klabu ya West Bromwich Albion imevunja rekodi ya klabu hiyo kwa kumsajili Winga wa Tottenham Spurs kwa kitita cha Pauni milioni 13. Chadli alijiunga na Spurs akitokea FC Twente kwa uhamisho wa pauni milioni 7 Julai 2013… Read More

0 comments:

Post a Comment